Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, November 29, 2016

ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA NA VIONGOZI WA DINI KATIKA UWANJA WA SIA

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Mkalla (kulia) akiwa ameambatana na wajumbe wa Kamati ya ulinzi na Usalama mkoa na viongozi wa dini ya Kikristo na Kiislamu mkoani Mbeya wakikagua Miundombinu ya Uwanja wa Ndegea wa Kimataifa wa Songwe(SIA).Lengo la ziara hii iliyofanyika jana ni kuwezesha wananchi kutambua jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuboresha Sekta ya Usafiri nchini

 Mkuu wa Usalama katika uwanja wa SIA Ole Laput akitoaa maelekezo juu ya masuala ya usalam uwanjani SIA
 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Mkalla akifafanua jambo kwa wajumbe alioongozanaa nao kwenye ziara ya kukagua uwanja wa SIA


 Mhariri Mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bw. Joachim Nyambo akikagua taa za kuongozea ndege wakati wa mchana kunapokuwa na ukungu.
 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Mkalla na wajumbe wengine wakisikiliza maelezo ya Uongozaji ndege kutoka kwa mhandisi Samweli Murembe aliyekuwa zamu kwenye Chumba cha kuongozea ndege
Juu ni Viongozi wa dini na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Mbeya wakiangalia namna tukio la uzimaji moto linavyofanyika iwapo kutatokea ajali ya ndege kuwaka moto ikiwa uwanjani.Chini ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Mkalla akishirikiana na viongozi wa dini kuuombea uwanja wa SIA


                              HABARI KAMILI

WAKAZI mkoani Mbeya wamehamasishwa kujiandaa na ujio wa Ndege za Kampuni ya ATC zinazotarajiwa kuanza safari za Dar es salaam na Mbeya kuanzia DDesemba 2 mwaka huu.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla ametoa hamasa hiyo alipofanya ziara na viongozi wa dini mkoani hapa kutembelea Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe(SIA) lengo likiwa ni kujinea jitihada zinazofanywa na Serikali za kuukamilisha uwanja huo.

Makalla amesema taarifa zilizothibitishwa kuwa ndege za ATC zitakuwa zikifanya safari kwa siku tano kwa juma ambapo  siku hizo ni Jumatatu,jumatano,ijumaa,jumamosi na jumapili.

Amesema ndege ndege itakuwa ikitoka Dar es salaam saa sita mchana na kufika Mbeya saa nane na kisha saa nane na nusu kuanza safari ya kurudi Dar es salaam.

Amesema kutokana na fursa hiyo wakazi wa mkoa wa Mbeya na maeneo ya jirani wanapaswa kujipanga kuhakikisha wanakuwa wanufaika wa kwanza kutokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi wanazoweza kuzifanya kupitia fursa hiyo

Aidha mkuu huyo wa mkoa pia amesisitiza adhma ya mkoa wa Mbeya kunufaika na uwanja wa SIA kwa wawekezaji kuzalisha na kusafirisha maua,matunda na mbogamboga kwenda nje ya nchi mara ndege za kimataifa zitakapoanza kutua kwenye uwanja huo.

Amewataja  viongozi wa dini kuwa moja ya kundi muhimu linaloweza kuwahamasisha wananchi kuutumia uwanja huo kwa manufaa huku akiwasisitiza pia kutumia nafasi walizonazo kuhubiri amani ili uwanja huo uweze kuwa katika hali ya usalama wakati wote.

Kwa upande wao viongozi wa Dini walioshiriki ziara hiyo,wameipongeza serikali kwa jitihada zake za ujenzi wa uwanja wa SIA hususani hatua ya kufunga Taa za kuongozea ndege wakati wa Ukungu wakisema zitasaidia kwa kiasi kikubwa safari za ndege kuwa za uhakika.


Wameisihi serikali kuendelea kushughulikia changamoto ya kufunga taa za kuongozea ndege wakati wa usiku ili kuwezesha ndege kuanza kufanya safari zake wakati wote wakisema itawezesha uwanja huo kutumika kwa tija zaidi.

No comments:

Post a Comment