Picha inayo-trend kwa sasa kwenye mitandao ya
kijamii ni ya Mrisho Ngasa na afisa habari wa Mbeya City Dismas Ten ambayo
inaashiria tayari nyota huyo wa zamani wa Yanga ameshakamilisha deal na
‘wagonga nyundo wa Mbeya’ Mbeya City.
Mwezi Septemba mwaka huu Ngasa alijiunga na Fanja FC
inayoshiriki ligi kuu nchini Oman (Oman Professional League) ikiwa ni wiki tatu
tu, baada ya kuvunja mkataba na klabu ya Free State Stars ya South Africa.
Nyota huyo wa zamani wa vilabu vya Kagera Sugar,
Yanga, Azam FC na Simba vyote vya VPL hajadumu Oman na hatimaye amerejea tena
nchini na kusajiliwa na klabu ya Mbeya City ambapo ataungana na kocha wake wa
zamani Kinna Phiri aliyemsajili kutoka Yanga kwenda Free State Stars kabla ya
kocha huyo kutimuliwa kufatia mfululizo wa matokeo mabovu.
Afisa habari wa Mbeya City Dismas Ten ame-post picha
kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa pamoja na Mrisho Ngasa na kuandika
maneno yanosomeka: “Mnapokamilisha jambo kutakiana heri ndio uungwana.
No comments:
Post a Comment