Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, August 3, 2016

WAWILI MBARONI KWA KUHIMIZA OPARESHENI UKUTA

JESHI la polisi mkoani Mbeya linawashikilia watu wawili wakikabiliwa na tuhuma za kusambaza Ujumbe wenye kuashiria kuhatarisha amani ya nchi kupitia mtandao wa simu hatua inayohusishwa na  Tukio la Oparesheni Ukuta lililopangwa na Chama cha Demokrasia na maendeleo(Chadema) lifanyike Septemba mosi mwaka huu.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Mbeya Dhahiri Kidavashari,wanaoshikiliwa ni pamoja na mkazi wa kata ya Isanga jijini Mbeya Moses Mwaifunga(28) na Meshaki Mgaya(28)mkazi wa Ileje mkoani Songwe.

Kadhalika kamanda Kidavashari amesema leo kuwa jeshi hilo linawatafuta watuhumiwa wengine Emma Kimambo na Moris Chanonga ambao amesema popote walipo wanapaswa kujisalimisha wenye katika vituo vya polisi vilivyopo jirani nao.

Anasema watuhumiwa hao wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Chadema,wamehusika kusambaza jumbe mbalimbali unaoashiria kutokubaliana na agizo la serikali la kukataza kufanyika kwa uparesheni Ukuta kwakuwa Jumbe wanazosambaza zinashinikiza wafuasi wa chama hicho kutokata tama bali wajitokeze kushiriki oparesheni hiyo.

Anasema zipo baadhi ya jumbe ambazo watu hao wameonesha nia ya kufanya Oparesheni Ukuta hata kabla ya kuwadia kwa siku iliyokuwa ikitajwa na Chadema yaani Septemba Mosi huku pia nyingine zikionesha wamedhamiria kufanya uhalifu wa aina mbalimbali ikiwemo kuchoma ofisi za Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Kamanda Kidavashari anaonya wafuasi wa Chadema na wananchi wengine kuepuka kusambaza jumbe zinazoonekana kukiuka miiko na maadili ya Utaifa na pale wanapotumiwa kabla ya kuzituma kwa watu wengine wazifute au kutoa taarifa kwa vyombo vya dola.

Amewataka wananchi kuhakikisha wanafuata sheria zilizowekwa na mamlaka huku akisisitiza kuwa hata maandiko matakatifu katika baadhi ya vitabu vya dini yanaeleza kuwa Kila Mamlaka inatoka kwa Mwenyezi Mungu.

No comments:

Post a Comment