Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, August 2, 2016

WAZIRI ATAKA MIZANI KWENYE NYAMA CHOMA

WAZIRI wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dk Charles Tzeba ameagiza wakala wa vipimo nchini(WMA) kuhakikisha mfumo wa matumizi ya vipimo vya Mizani unazifikia huduma za za kijamii zote ikiwemo nyama choma.

Dk Tzeba ametoa agizo hilo jana alipokuwa akifungua Maonesho ya Wakulima ya Nanenane kanda ya Nyanda za Juu Kusini yanayofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya na kuhuduriwa na wadau kutoka Halmashauri za mikoa saba ya kanda hiyo.

Alisema miongoni mwa wateja wasionufaika na kile wanachonunua kutokana na kutojua ni kwa kiasi gani wamehudumiwa ni walaji wa nyama hususani zinazochomwa kwakuwa wauzaji hutumia njia ya kukadiria badala ya kuwapimia.

Alisema jambo la kushangaza ni kuwa wauzaji hao wa nyama choma huchukua bidhaa hizo kwenye bucha na machinjio zikiwa zimepimwa lakini wao hawataki kuwatendea haki wateja wao kwa kuwapimia kwa kipimo kinachotakiwa.

“Mteja wa nyamachoma anakadiriwa kwa vipande vya nyama anapewa bei,wakati muuzaji huyu wa nyama choma anaponunua dukani au machinjioni hakubali kutopimiwa.Hapa mteja anaibiwa”

“Lazima mteja ajue ni kiasi gani cha nyama amelipia kiasi cha fedha anachotajiwa.Suala la mazungumzo ya bei lije badae lakini tujue mteja anakula kiasi gani.Na hii yote inatokana na wakala wa vipimo kutotimiza wajibu wake” alisisitiza Tzeba.

Aliitaka WMA kuhakikisha inasimamia kwa uhakika mfumo wa matumizi wa vipimo vinavyotakiwa katika maeneo yote ikiwemo kwenye masoko ya bidhaa kama kuku,nyanya na vitunguu akisema bado mfanyabiashara ananeemeka kwa kuwanyoka wakulima na wateja wake.

Alisema serikali haiku tayari kuona vipimo vya makopo na ndoo vikiendelea kutumika bali kila mtanzania anapaswa awajibike kwa kuhakikisha kwenye eneo lake matumizi ya vipimo sahihi yanazingatiwa ili kuleta usawa katika uchumi.

No comments:

Post a Comment