WAZIRI wa Kilimo,Mifugo
na Uvuvi Dk Charles Tzeba ameagiza wakala wa vipimo nchini(WMA) kuhakikisha
mfumo wa matumizi ya vipimo vya Mizani unazifikia huduma za za kijamii zote
ikiwemo nyama choma.
Dk Tzeba ametoa agizo
hilo jana alipokuwa akifungua Maonesho ya Wakulima ya Nanenane kanda
ya Nyanda za Juu Kusini yanayofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini
Mbeya na kuhuduriwa na wadau kutoka Halmashauri za mikoa saba ya kanda hiyo.
Alisema miongoni mwa
wateja wasionufaika na kile wanachonunua kutokana na kutojua ni kwa kiasi gani
wamehudumiwa ni walaji wa nyama hususani zinazochomwa kwakuwa wauzaji hutumia
njia ya kukadiria badala ya kuwapimia.
Alisema jambo la kushangaza
ni kuwa wauzaji hao wa nyama choma huchukua bidhaa hizo kwenye bucha na
machinjio zikiwa zimepimwa lakini wao hawataki kuwatendea haki wateja wao kwa
kuwapimia kwa kipimo kinachotakiwa.
“Mteja wa nyamachoma
anakadiriwa kwa vipande vya nyama anapewa bei,wakati muuzaji huyu wa nyama
choma anaponunua dukani au machinjioni hakubali kutopimiwa.Hapa mteja anaibiwa”
“Lazima mteja ajue ni
kiasi gani cha nyama amelipia kiasi cha fedha anachotajiwa.Suala la mazungumzo
ya bei lije badae lakini tujue mteja anakula kiasi gani.Na hii yote inatokana
na wakala wa vipimo kutotimiza wajibu wake” alisisitiza Tzeba.
Aliitaka WMA
kuhakikisha inasimamia kwa uhakika mfumo wa matumizi wa vipimo vinavyotakiwa
katika maeneo yote ikiwemo kwenye masoko ya bidhaa kama kuku,nyanya na vitunguu
akisema bado mfanyabiashara ananeemeka kwa kuwanyoka wakulima na wateja wake.
Alisema serikali haiku tayari
kuona vipimo vya makopo na ndoo vikiendelea kutumika bali kila mtanzania
anapaswa awajibike kwa kuhakikisha kwenye eneo lake matumizi ya vipimo sahihi
yanazingatiwa ili kuleta usawa katika uchumi.
No comments:
Post a Comment