MAHAKAMA ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya
imewahukumu kutumikia kifungo cha maisha jela vijana wawili wakazi wa wilayani
Chunya mkoani hapa kutokana na kosa la ubakaji wa mwanamke mmoja waliyembaka
mbele ya watoto wake.
Kadhalika mahakama hiyo imewahukumu vijana hao
wawili kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kutokana na kosa la Unyang’anyi wa
kutumia silaha ambapo siku ya tukio walimjeruhi mume wa mwanamke waliyembaka.
Vijana waliokumbwa na vifungo hivyo viwili kutokana
na mashitaka mawili yaliyokuwa yakiwakabili ni Ngaru Joseph(32) na Pili Mneme
Kapigi(30) wote wakiwa ni wakazi wa wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Awali ilielezwa mahakamani hapo na Mwendesha
mashitaka wa Jeshi la Polisi Mazoya Luchagula, Mbele ya hakimu mfawidhi wa
mahakama hiyo Alice Mkasela kuwa mnamo Julai 10 mwaka huu majira ya saa nane
usiku nyumbani kwa mlalamikaji katika kijiji cha Ukwavila wilayani Mbarali washitakiwa
walivamia na kuvunja mlango nyumba ya mkazi huyo aliyekuwa amelala na mke na
watoto wao.
Luchagula alisema walipo fanikiwa kuingia ndani ya
nyumba hiyo washitakiwa hao walimjeruhi baba wa familia kwa kumkata na shoka
kichwani kisha wakapora fedha kiasi cha
shilingi 580,000 wakachukua nguo zote za wanafamilia na kisha kumbaka mama wa
familia mbele ya mumewe na watoto.
Mwendesha mashitaka huyo alisema wanafamilia hao kupitia
mwanga wa taa ya sola waliweza kuwatambua watuhumiwa kabla wazazi hawajapelekwa
hospitali ya misheni Chimala walikolazwa kwaajili ya matibabu.
Kufuati makosa hayo Luchagula aliiomba mahakama
kutoa adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine walio na
tabia hizo wilayani hapa na kwingineko nchini.
Akito adhabu kwa washitakiwa,hakimu Mkasela
aliyesema ameridhishwa na ushauhi uliotolewa mahakamani hapo na pande zote
mbili alisema kwa kosa la kwanza la Unyangaji wa kutumia Silaha washitakiwa
watakapswa kutumikia kifungo cha miaka 30 jela na kwa kosa la pili la ubakaji
watatumikia kifungo cha maisha jela ili iwe fundisho kwao na watu wengine.
Awali washitakiwa waliiomba mahakama kuwapunguzia
adhabu wakisema bado umri wao ni mdogo na wanategemewa na familia zao,maombi
ambayo yalitupiliwa mbali na hakimu Mkasela.
No comments:
Post a Comment