AJALI YATOKEA ILOLO MBEYA
Gari
aina ya Canter Toyota ikiwa imetumbukia katika mto Jianga maeneo ya
Ilolo Jijini Mbeya, baada ya kuvunjika kwa daraja na katika ajali hiyo
hakuna mtu aliyejeruhiwa. Lakini wakazi wa eneo hilo walieleza kwamba
daraja hilo ni bovu toka muda mrefu na viongozi wao hawajafanya jitihada
zozote juu ya ubovu huo.
Mmmh jamani hatari
Wakazi wa eneo la jirani na tukio la ajali waliofika kudhuhudia tukio hilo.
Hata
hivyo kufuatia tukio hili,Kata za Ilemi,Sinde na Isanga zinapaswa
kukutana katika meza moja ya mazungumzo kwa ajili ya kujenga daraja hilo
ambalo ni kiunganishi cha kila pande na mara nyingi limekuwa likitumiwa
na wagonjwa kwenda Kituo cha Afya cha Mwanjelwa na katika shughuli
mbalimbali za kitaifa za kimaendeleo.
( picha na Godfrey Kahango).
No comments:
Post a Comment