Mwandishi wa Blogu hii ya kijamii ya Lyamba Lya Mfipa kutoka mji mdogo wa Tunduma Azaria Mwanyika,anaripoti kuwa
Mwanaskauti na pia mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari mwalimu
J.K.Nyerere iliyopo wilayani Momba katika mji mdogo waTunduma
aliyejulikana kwa jina la Boazi Essau Mwalusanya amejinyonga hadi kufa.
Sababu za kujinyonga kwake hazijajulikana mpaka sasa. kabla ya
kujinyonga mwanafunzi huyo alikuwa akiongea lugha mbalimbali ikiwemo
lugha ya Kiarabu na alikaliliwa akisema atakufa mwezi wa sita na kudai
kuwa atakumbukwa kama msanii maarufu aliyekufa hivi karibuni kwa
mtikisiko wa ubongo. mwanafunzi huyo amezikwa tarehe 6/6/2012 katika
makaburi ya migimbani mjini Tunduma.
Wakati huo huo kumetokea fujo (timbwili) kubwa katika
shule hiyo kwa wanafunzi kuchomana visu, shule hiyo imekuwa ikijihusisha
na mikasa mbalimbali hasa ya utovu wa nidhani ikiwemo uvutaji bangi
hivyo kuwapa wakati mgumu walimu wao katika shughuli za ufundishaji.
No comments:
Post a Comment