Kamanda Diwani ameyasema hayo leo(JUNI 11) alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake ikiwa ni kikao chake cha kwanza kukifanya na
wana tasnia hiyo tangu alipohamishiwa mkoani hapa.
Amekiri mkoa wa Mbeya kuwa miongoni mwa
mikoa nchini ambayo majina yake hayatajwi vizuri kutokana na kukithiri kwa
vitendo vya uharifu hali aliyosema ni changamoto kwake kuandaa mikakati
madhubuti itakayourejesha mkoa katika hali ya amani na utulivu.
Amevitaja vitendo vya upigaji nondo kuwa
miongoni mwa vile vinavyouchafua mkoa na kuahidi kuwa mikakati ya kuwabana wale
wote wanaohusika na vitendo hivyo upo tayari na kinachofuata sasa ni
utekelezaji.
No comments:
Post a Comment