Timu ya taifa ya wanawake ya Ethiopia imeifunga Twiga Stars ya Tanzania goli 1-0 katika mchezo wa marudiano kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Nane za Afrika
kwa Wanawake (AWC) zitakazofanyika Novemba mwaka huu nchini Equatorial
Guinea uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni leo.
Katika matokeo ya mechi ya awali Twiga Stars ilifungwa mabao
2-1 na na sasa timu ya Ethiopia imefuzu kucheza fainali hizo za Equatorial Guinea.
Nchi ambazo tayari zimefuzu kwa fainali hizo ni wenyeji Equatorial Guinea na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
KIKOSI CHA TIMU YA TAIFA YA WANAWAKE YA ETHIOPIA
No comments:
Post a Comment