WATU watatu wasiofahamika majina wala
makazi wamemteka mchungaji wa kanisa la Asemblies Of God (TAG) la Iyunga jijini Mbeya na kumpora fedha taslimu
za kanisa kiasi cha shilingi milioni 4 laki 9 na 3000.
Msemaji wa jeshi la polisi mkoani Mbeya
Majaliwa Mbogela amemtaja mchungaji huyo kuwa ni Husein Enock(40) mkazi wa
Iyunga na kuwa amekutwa na mkasa huo Juni 5 mwaka huu majira ya saa 8:00 za
mchana alipotoka kuchukua fedha hizo katika tawi la benki ya Biashara ya Afrika
(CBA) lililopo mwanjelwa jijini hapa.
Mbogela amesema baada ya mchungaji Enock
kutoka nje ya benki hiyo alikuta gari aina ya Noah yenye namba asiyoifahamu na ndani yake
kulikuwa na watu watatu aliokuwa akiwafahamu kwa sura na ndipo wakampa msaada
wa rifti kwenda kanisani kwake Iyunga.
Tofauti na matarajio ya mchungaji huyo,dereva
wa gari hiyo baada ya kuingia barabara kuu alielekea mwelekeo tofauti wa kwenda
mkoani Iringa na walipofika katika eneo la Mlima Nyoka nje kidogo ya jiji la
Mbeya walimnyang’anya fedha zote na kumtelekeza hapo kisha wao wakatoweka.
No comments:
Post a Comment