OFISI YA BENKI YA POSTA TANZANIA TAWI LA MBEYA LILILOPO JIRANI NA OFISI ZA NSSF NA SUMATRA JIJINI MBEYA
WAKIANGALIA UJUMBE WA KILA ANAYECHANGIA DAMU NI SHUJAA ULIOANDIKA KWEENYE TISHETI HIZO
HAPA MAOFISA HAO WAKIFURAHIA KWA PAMOJA MSAADA ULIOTOLEWA
MENEJA WA BENKI YA POSTA BWANA JULIUSA AKIFAFANUA JAMBO JUU YA HUDUMA ZINAZOTOLEWA NA BENKI HIYO BAADA YA KUKABIDHI MSAADA
XXXXXXXXXXXXXXXX HABARI KAMILI XXXXXXXXXXXX
BENKI
ya posta nchini tawi la Mbeya leo(Juni5) imekabidhi msaada wa tisheti 150 wenye
thamani ya shilingi milioni mbili kwa kituo cha Mpango wa Taifa wa Damu salama
kanda ya Nyanda za juu kusini.
Kutolewa
kwa msaada wa tisheti hizo zilizo na nembo ya kaulimbiu ya maadhi misho ya damu
salama mwaka huu ya KILA MCHANGIAJI DAMU NI SHUJAA kumelenga kusaidia hamasa
kwa wadau kuchangia damu.
Akikabidhi
msaada huo,meneja wa benki ya Posta tawi la Mbeya Hamphrey Julius amesema kutoa
msaada huo kunatokana na benki kutambua kuwa ni taasisi ya umma inayopaswa
kurejesha faida kidogo inayopata kwa wananchi ambao ndiyo wamiliki kupitia
uchangiaji huduma za kijamii.
Naye
Afisa utumishi wa kituo hicho cha damu salama Kundael Saria amesema msaada huo
umewafikia kwa wakati na kuwaomba wadau wengine kuiga mfano huo ili kuwezesha
hamasa ya uchangiaji damu.
Saria
amesema kituo hicho kinategemea nguvu ya wadau mbalimbali katika kuendelea
kutoa hamasa ya uchagiaji damu kwa hiari hasa kutokana na ufinyu wa bajeti yake
katika kila mwaka wa fedha
No comments:
Post a Comment