Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, June 28, 2012

MADAKTARI MBEYA WATIMULIWA

BODI ya hospitali ya Rufaa ya Mbeya imechukua uamuzi wa kuwatimua madaktari 54 waliokuwa katika mafunzo na wengi 18 wa kuajiriwa waliokuwa katika mgomo.

Mwenyekiti wa bodi hiyo kaimu mkuu wa mkoa wa Mbeya dk.Norman Sigalla alitangaza uamuzi huo leo hii (Juni 28) katika kikao kilichowakutanisha wajumbe wa bodi na waandishi wa habari.

Dk.Sigalla amesema bodi imefikia maamuzi hayo baada ya madaktari kushindwa kutimiza wajibu wao ikiwa ni pamoja na kutofika katika kikao walichoitwa na pia kutojibu barua walizopewa na kutakiwa kujibu ni kwa nini wasiwajibishwe.

Amesema kutofika kazini kwa madaktari hao kwa siku tano mfululizo walivunja mkataba wao kwa mujibu wa kanuni za kudumu za utumishi wa umma toleo la mwaka 2009 kifungu namba F16,F 17 na F 27.

Amesema kwakuwa bodi ndiyo huingia mkataba na madaktari hao,imechukua uamuzi wa kuvunja mikataba nao na kuwarejesha kwa muajiri wao yaani waziri wa Afya na Ustawi wa jamii ili naye achukue hatua za juu zaidi.

Amefafanua kuwa wameshatoa agizo la kuwataka madaktari hao waliokuwa katika mafunzo kuondoka katika hosteli waliyokuwa wakiishi kwa gharama za hospitali ya rufaa.

Lyamba Lya Mfipa imefika katika hosteli ya madaktari hao saa  tisa alasiri na kukuta wakiendelea na harakati za kuhamisha mali zao kutoka katika hosteli hiyo na kuelekea mitaani.

Wakati huo huo mwenyekiti wa shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi (TUCTA) Nicholaus Mgaya akizungumza na waandishi wa habari mapema leo jijini Mbeya amelaani namna inayotumiwa na madaktari kutafuta suluhu ya madai yao.

Alisema yawezekana madai yao ni ya msingi lakini walipaswa kutumia njia ya mazungumzo na hasa kup[itia chama cha wafanyakazi cha TUGHE walicho wanachama na si chama cha kitaaluma wanachokitumia.

No comments:

Post a Comment