WALIMU
waliozoea kuwapa chaki na notsi wanafunzi ili wakawaandikie wenzao madarasani sasa
watawajibishwa na wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi watakapobainika.
Naibu
waziri wa wizara hiyo Filipo Mulugo ametoa agizo hilo katika mkutano wake na viongozi mbalimbali wa idara ya elimu
kanda,mkoa na wilaya pamoja na wakuu wa shule za sekondari za mkoani Mbeya na
wakuu wa shule za msingi katika halmashauri ya jiji.
Kadhalika
Mulugo amekataza mamonita wa madarasa kuitisha majina ya mahudhurio ya wanafunzi
wenzao akisema mwenye jukumu hilo ni mwalimu wa darasa husika na itakapobainika
mwalimu huyo pamoja na mkuu wa shule husika watawajibishwa.
Amesema
shughuli zote hizo si za mwanaafunzi na zinazorotesha ufanisi katika utendaji
kwakuwa walimu wanakaimisha majukumu hayo na wao wakibaki wanapiga soga ofisini
mwao na walimu wenzao.
No comments:
Post a Comment