Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, July 19, 2012

WAHIMIZWA KUHAMASISHA SENSA


VIONGOZI wa dini,vyama vya siasa na asasi mbalimbali za kiserikali na
binafsi wametakiwa kushiriki katika kutoa hamasa itakayowezesha
kufanikishwa kwa zoezi la sense ya watu na makazi linalotarajiwa
kufanyika agosti 26 mwaka huu.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro alitoa mwito huo alipokuwa akifungua semina ya siku 12 inayolenga kutoa mafunzo kwa
wasimamizi wa sense watakaokwenda kuwafundisha makarani katika kata za
wolaya zilizopo mkoani hapa.

Kandoro alisema viongozi hao wanayo nafasi kubwa ya kutoa elimu juu ya
umuhimu wa sense ya watu na makazi kwa jamii wanazozihudumia hivyo
wakiwajibika ipasavyo watakuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha
zoezi hilo.

Aliwaomba kutumia fursa walizonazo kuwaelimisha wananchi juu ya
umuhimu huo ikiwa ni pamoja na kuiwezesha serikali kuwa na takwimu
sahihi zitakazosaidia kuwa na mipango ya kimaendeleo inayoendana na
hali halisi ya mahitaji iliyopo nchini.

Aliwataja wanahaabari kupitia vyombo vyao kuwa mchango mkubwa na
muhimu unaohitajika pia katika kutoa elimu juu ya Sensa pamoja na
kuufahamisha umma juu ya njia mbalimbali zitakazotumika na ni jinsi
gani taarifa zitakazotolewa na wananchi zitabaki kuwa siri.

Aliwataka wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha pale makalani
watakapofika katika familia zao na kuhitaji taarifa mbalimbali
kutokana na kumbukumbu alizosem,a pia wanapaswa waziandae ili
kurahisisha mahojiano baina yao.

Mkuu huyo wa mkoa aliwataka washiriki wa semina hiyo kuhakikisha
wanakuwa makini kwenye mafunzo ya nadharia na vitendo wanayopewa ili
baadaye waende kuwa walimu wazuri kwa wenzao watakaokwenda
kuwafundisha kwenye kata za wilaya wanazotoka.

Alisema ni vema wakatambua kuwa taifa limewaamini na kuwapa dhamana
kubwa likiwa na imani kuwa watatekeleza wajibu wao kwa
umakini,uadirifu na uaminifu mkubwa ili lipate takwimu zilizo sahihi.

“Nina imani hamkupendelewa,mliteuliwa kutokana na sifa mlizonazo.Vivyo
hivyo na taifa linategemea mtafanya vile linavyohitaji.Zoezi hili
linaigharimu serikali pesa nyingi lakini ni muhimu na ndiyo maana
limekuwa likifanyika kila baada ya miaka kumi” alisema

Alisema miaka yote zoezi kama hilo limekuwa likifanyika vizuri lakini
mwaka huu linapaswa lifanyike vizuri zaidi huku akiwatoa wasiwasi
wananchi kuwa shughuli za kimaendeleo na kijamii hazitaathiriwa na
kufanyika kwa zoezi la Sensa kwakuwa zitaendelea kama kawaida.

Awali Mratibu wa Sensa mkoa wa Mbeya Theresia Lyimo alisema mafunzo
hayo yanahudhuriwa na washiriki 249 ambapo 244 kati yao wanatoka
wilaya za mkoani hapa na watano ni kutoka mkoani.

No comments:

Post a Comment