Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, July 19, 2012

RC AAGIZA MGAANGA WA JADI KUKAMATWA

KAMATI ya ulinzi na usalama wilayani Mbarali mkoani Mbeya imeagizwa kumsaka mganga wa jadi anayetajwa kuwapotosha wananchi katika kata ya Ruiwa na kusababisha kuwazika watuhumiwa wa uchawi wakiwa hai.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro alitoa agizo hilo katika kikao maalumu cha baraza la madiwani wilayani Mbarali kilicholenga kujadili taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali(CAG).

Kandoro alisema katika kata hiyo tayari yalitokea mauaji ya mkazi mmoja aliyezikwa kwa kufukiwa kaburini akiwa hai na tukio la pili ilikuwa azikwe chifu wa eneo hilo ajulikanaye kama chifu Merere lakini akaokolewa na askari wa jeshi la polisi.

Alisema matukio ya mauaji hayo ynaelezwa kusababishwa na mganga mmoja wa jadi aliyehamia kwenye kata hiyo akitokea wilayani Mbozi ambaye amekuwa akipiga ramli na kuwatuhumu baadhi ya wakazi kuwa wasababishi wa vifo vya watu ndani ya vijiji vya kata hiyo.

Kufuatia maoni yam ganga huyo wakazi wamekuwa wakijichukulia sheria mikononi kwa kuwazika hai watuhumiwa pasipo ushahidi wowote wa kisheria na wala maamuzi kutoka vyombo vya dola.

Akizungumzia hali hiyo mkuu wa mkoa alisema ni lazima kamati ya ulinzi imtafute mganga huyo na kumkamata na kuhakikisha inampa taarifa haraka iwezekanavyo.

Alisema jamii inahitaji amani na utulivu ili ijishughulishe na shughuli za kimaendeleo hivyo kuwepo kwa mtu anayechochea upotevu wa amani hauwezi kuvumiliwa hivyo ni lazima mganga huyo achukuliwe hatua.

Alisema waganga kama hao hawahitajiki mkoani hapa kwakuwa badala ya kuisaidia jamii kuondokana na matatizo wanasababisha migogoro inayowaingia wananchi katika hali hataari kwa amani waliyo nayo.

No comments:

Post a Comment