MAANDALIZI YA SIKU YA MASHUJAA JULAI 25
Siku
ya Mashujaa nchini Tanzania inaadhimishwa kesho Julai 25 ambapo Majeshi ya
Ulinzi na Usalama yatakuwa yakiwakumbuka mashujaa wa Tanzania waliofariki kwa
ajili ya kulipigania taifa hili,pia kwenye vita kuu ya pili ya Dunia.
Kitaifa yataadhimishwa mkoani
Dar es Salaam ambapo wito umetolewa kwa wakazi wa Jiji hilo kujitokeza katika
maadhimisho hayo huku mgeni rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
na Amir Jeshi Mkuu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Mkoani Mbeya mapema leo asubuhi
maandalizi kwa ajili ya siku hiyo yamefanyika katika viunga vya Jiji la Mbeya
karibu na eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa.
No comments:
Post a Comment