Mwenyekiti
wa TLCO Kura Mayuma alikitambulisha chama hicho leo(Julai 8) kwa waandishi wa
habari na kuthibitisha kuwa tayari kimesajiriwa na msajiri wa vyama vya hiari
tangu Juni 26 mwaka huu na kupata cheti namba S.A.18225.
Mayuma
amesema changamoto zinazowakabili wakandaarasi nchini ndizo zilipelekea wakae
na kuona umuhimu wa kuwa na chombo kama hicho wakiamini kitakuwa na nguvu ya
kweli ya kutatua matatizo yao.
Amesemaa
chama hicho kitawaunganisha wakandarasi ili kupigania haki zao na kuwa na sauti
moja ya kuiomba serikali iweze kuwathamini vya kutosha kama wazawa wanaotoa
mchango mkubwa kwenye fani ya miuondombinu.
Amesema
pia kitawawezesha weakandarasi wenyewe kuungana na kuweza kusaidiana wenyewe
badala ya kuoneana wivu na kukosa mshikamano hivyo chama kitaweza kumaliza
matatizo baina yao ama wao na waajiri kwa hatua za awali.
Ameongeza kuwa
TLCO pia itapigania usawa kwenye upatikanaji wa kazi akisema kwa muda mrefu
kumekuwepo na tatizo kubwa kwamba wakandarasi wazawa kunyimwa kazi na serikali
yao kwa hisia na visingizio mbalimbali ikiwemo ukosefu wa mitaji na kuwajali
kwa kuwaamini zaidi wanaotoka nje.
No comments:
Post a Comment