MKUU
wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amewata wakazi jijini hapa kutambua kuwa watendaji wanaosema
anashindwa kumwajibisha mkurugenzi wa jiji Juma Iddy kwakuwa na ndugu yake ni
wapotoshaji.
Kandoro
aliyasema hayo ktika kikao maalumu cha baraza la madiwani kilicholenga kujadili
taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali (CAG) na kubainisha kuwa
wapo baadhi ya watendaji wanaozusha undugu kati yake na mkurugenzi wakati hata
kwao hakufahamu.
Alisema
watendaji hao wamefikia hatua ya kumuandikia barua wakimtaka amwajibishe licha
ya kuwa ni ndugu yake wakidai utendajikazi wake una kasoro nyingi.
Alisema
kwa uchunguzi alioufanya ametambua kuwa watendaji hao ni wale ambao awali
waliigeuza halmashaueri hiyo kama shamba la bibi na kuiba kwa kadiri
walivyoweza lakini hivi sasa mianya hiyo imezibwa.
Alisema
kutokana na kukosa nafasi ya kuiba ndiyo maana wanamchukia mkurugenzi huyo
kwakuwa wanaamini tangu afike wameshindwa kuendelea na tabia yao mbayo ya
kutafuna bila aibu fedha za serikali.
Alisema
yawezekana kweli mkurugenzi huyo akawa na mapungufu yake lakini serikali ina
nufaika kwa kiasi kikubwa kwa uwepo wa mkurugenzi huyo kutokana na ukali wake
kwenye kutetea fedha za umma.
Alimtaka
mkurugenzi huyo kuendelea na kasi hiyo akisema serikali inahitaji watu wa namna
hiyo wanaochukiwa na wezi kwakuwa wanadhibiti mianya inayoweza kutumiwa na
wachache kujinufaisdha kwa fedha za maendeleo ya walalahoi.
No comments:
Post a Comment