MKUU
wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro ametoa muda wa siku mbili kwa mkuu wa wilaya ya
Chunya kutoa taarifa juu ya upotevu wa nyaraka zenye taarifa ya miradi ya
kilimo zilizopotea.
Kwa
mujibu wa Kandoro nyaraka hizo zinazoelezwa kupotea ni za miradi ya kilimo
yenye thamani ya jumla ya shilingi 408,659,706.
Katika
kikao maalumu cha baraza kilicholenga kujadili taarifa ya mdhibiti na mkaguzi
wa fedha za serikali(CAG) mkuu wa mkoa amehoji ni kwa nini nyaraka hizo zipotee
na hakuna hatua zilizochukuliwa.
Amesema
upo uwezekano mkubwa wa kuwa fedha hizo hazikutumika ipasavyo na ndiyo maana
zimefichwa ili ukweli usibainike.
“Kwa
nini zipotee?Inaonekana kuna shughuli hazikufanyika lakioni fedha
zilitumika.Nataka ndani ya wiki hii nipate maelezo juu ya upotevu huo na
ilikuwaje.Mkuu wa wilaya hakikisha mpaka alhamisi ya wiki hii uwe umeniletea
maelezo ofisini kwangu na hawa madiwani wapewe taarifa kamili” alisisitiza.
Amezidi
kuitaja idara ya kilimo kuwa na mapungufu makubwa katika utendaji wake kutokana
na taarifa mbalimbali zinazobainisha kuwepo kwa kasoro.
Mkuu
huyo wa mkoa amesema pia kuna miradi ya kilimo ya kiasi cha shilingi 496
milioni haijakamilika licha ya serikali kutoa fedha zote na kuhoji ni kwa nini
lakini swali hilo halikupata majibu kutokana na afisa kilimo wa halmashauri ya
wilaya hiyo kutohudhuria kikao hicho.
Aliendelea
kusema kuwa pia ipo miradi yenye thamani ya shilingi milioni 73 haijakamilika
na kuhoji kuna nini katika idara ya kilimo mpaka kuwe na uozo wa namna hiyo.
Aliwataka
madiwani kutokubali kuburuzwa na wakuu wa idara na kukubali kupitisha taarifa
za miradi kwenye vikao vyao pasipo kujiridhisha iwapo zinaendana na uhalisia wa
miradi husika.
Kandoro
pia amezishushia rungu idara za Maji, na Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF)akisema
pia zinatuhumiwa kwa kuwa na uozo wa matumizi mabovu ya fedha kama ilivyo
kwenye kilimo na kuhitaji maelezo ya kina ni kwa nini.
Amesema
katika idara ya maji kuna kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 4.6 zimetumika pasipo maelezo ya matumizi yake
huku pia kiasi cha zaidi ya milioni tano zikionekana kuwa malipo ya kughushi.
Kwa
upande wa TASAF amesema kuna kiasi cha zaidi ya shilingi 5020,000 zimetumika
kununua mafuta lakini hakuna nyaraka zinazoelekea mafuta yalinunuliwaje na
kutumika vipi.
No comments:
Post a Comment