Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, July 25, 2012

POWERTILLER 40 HAZITUMIKI CHUNYA


MATREKTA madogo(Powertiller) 40 yaliyonunuliwa na halmasahauri ya wilaya ya Chunya na kusambazwa vijijini hayafanyi kazi.

Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya hiyo Deodatus Kinawiro matrekta hayo yaliyoigarimu serikali zaidi ya shilingi milioni 217 hayajafanya kazi yoyote tangu yapelekwe vijijini ikiwa ni zaidi ya mwaka sasa umepita huku sababu za kutotumika zikiwa hazifahamiki.
 
Kinawiro aliyasema hayo katika kikao maalumu cha baraza la madiwani kilicholenga kujadili taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali(CAG) kilichokuwakikiongozwa na mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro.

Aliyasema hayo kufuatia mkuu wa mkoa kuhoji iwapo matrekta yanayotajwa katika moja ya hoja za CAG kwenye taarifa yake ya mwaka wa fedha 2010/2011 kuwa mpaka ukaguzi unafanyika matrekta hayakuonekana licha ya fedha kutumika na ndipo madiwani wakajibu kuwa yalinunuliwa na kusambazwa vijijini.

Hata hivyo mkuu wa wilaya aliwashangaa madiwani haoa kisema hawasemi ukweli juu ya matumizi ya matrekta hayo kwani hayafanyi shughuli iliyolengwa na serikali ya kuwapunguzia wakulima adha ya kulima kwa mkono.

Kinawiro alitolea mfano katika kata ya Ifumbo kuliko na mradi mkubwa waumwagiliaji akisema zilipelekwa Powertiller nne na tatu kati ya hizo zimeendelea kukaa bila matumizi na moja inatumiwa kwa shughuli za kubeba mchanga na mawe na si kulimia.

Alisema kama serikali ya wilaya tayari wamemuandikia barua mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ili aeleze ni kwa nini powertiller hizo hazijaanza kuwasaidia wakulima kama maelekezo ya serikali yanavyoeleza.

Alisema pia serikali kuu imepeleka fedha kwaajili yakununua powertiller nyingine kumi lakini amezuia ununuzi huokwakuwa 40 za kwanza hazijaonekana kufanya chochote.

“Tunalazimika kuhoji zile za awali hazifanyi kazi mpaka sasa kuna haja gani ya kununua nyingine 10.Tumeiuliza halmashauri na sasa tunasubiri majibu kutoka kwa mkurugenzi” alisema.

No comments:

Post a Comment