Kamanda wa polisi
mkoani Mbeya Athuman Diwani alisema watuhumiwa wa makosa hayo
wamekamatwa katika oparesheni maalumu ya kupambana na uharifu iliyoanza Juni 8
mwaka huu na hayo ni matokea ya hadi usiku wa kuamkia leo (juni 25).
Kamanda Amesema
katika matukio ya wizi wa diseli jumla ya lita 4,440 zenye thamani ya zaidi ya
shilingi laki tisa zilikamatwa na tayari mahakama imeamuru mafuta hayo
yarejeshwe yalikoibwa ili yakaendeleze shughuli za ujenzi wa barabara huku
watuhumiwa nane wa wizi huo wakiwa tayari wamefikishwa mahakamani.
Amewataja
watuhumiwa hao kuwa ni Lusekelo Paza,Anyemike Swile,Weiti Mwakatumbula,Michael
Mwampamba,Mahona John,Erasto Mwaipaja,Seleman Nasoro na Hassan mrisho.
Amesema katika
oparesheni hiyo pia zimekamatwa pikipiki tatu zilizoibwa akizitaja kuwa ni
yenye namba T 584 BPU aina ya Star,T 301 BRU aina ya SanLG na T 489 BQU aina ya
Sanya.
Mali nyingine ni bunduki
mbili zilizotengenezwa kienyeji zinazotumia risasi za Shotgu,risasi nane,Televisheni
mbili,kompyuta ndogo(Laptop) mbili,Printa moja,redio tatu,mbili aina ya Sub ufa
na moja ya kawaida pamoja na simu nane za aina mbalimbali.
Hata hivyo amesema
matokeo hayo mazuri yanatokana na ushirikiano mzuri ulioneshwa kati ya raia
wema na askari wa jeshi hilo akisema wananchi walijitahidi kwa kiasi kikubwa
kutoa taarifa juu ya uwepo wa vitendo vya uharifu.
Amewaomba wananchi
kuendeleza ushirikiano huo mzuri akisema utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza
uharifu na kuufanya mkoa kuwa na amani na utulivu.
No comments:
Post a Comment