Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, June 25, 2012

88 MBARONI KWA UHARIFU MBEYA

WATU 88 wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani hapa kwa kuhusika na matukio mbalimbali ya uharifu ikiwemo wizi wa mafuta aina ya diseli kwaajili ya kuendeshea mitambo katika ujenzi wa barabara kati ya Tunduma-Sumbawanga.

Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Athuman Diwani alisema watuhumiwa wa makosa hayo wamekamatwa katika oparesheni maalumu ya kupambana na uharifu iliyoanza Juni 8 mwaka huu na hayo ni matokea ya hadi usiku wa kuamkia leo (juni 25).

Kamanda Amesema katika matukio ya wizi wa diseli jumla ya lita 4,440 zenye thamani ya zaidi ya shilingi laki tisa zilikamatwa na tayari mahakama imeamuru mafuta hayo yarejeshwe yalikoibwa ili yakaendeleze shughuli za ujenzi wa barabara huku watuhumiwa nane wa wizi huo wakiwa tayari wamefikishwa mahakamani.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Lusekelo Paza,Anyemike Swile,Weiti Mwakatumbula,Michael Mwampamba,Mahona John,Erasto Mwaipaja,Seleman Nasoro na Hassan mrisho.

Amesema katika oparesheni hiyo pia zimekamatwa pikipiki tatu zilizoibwa akizitaja kuwa ni yenye namba T 584 BPU aina ya Star,T 301 BRU aina ya SanLG na T 489 BQU aina ya Sanya.

Mali nyingine ni bunduki mbili zilizotengenezwa kienyeji zinazotumia risasi za Shotgu,risasi nane,Televisheni mbili,kompyuta ndogo(Laptop) mbili,Printa moja,redio tatu,mbili aina ya Sub ufa na moja ya kawaida pamoja na simu nane za aina mbalimbali.

Hata hivyo amesema matokeo hayo mazuri yanatokana na ushirikiano mzuri ulioneshwa kati ya raia wema na askari wa jeshi hilo akisema wananchi walijitahidi kwa kiasi kikubwa kutoa taarifa juu ya uwepo wa vitendo vya uharifu.

Amewaomba wananchi kuendeleza ushirikiano huo mzuri akisema utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uharifu na kuufanya mkoa kuwa na amani na utulivu.

No comments:

Post a Comment