WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) wametakiwa kutochagua viongozi kwa nafasi zao za kifedha wanazozitumia kurubuni wananchi kwa kutoa misaada mingi.
Katibu wa Itikadi
na Uenezi wa CCM Nape Nnauye alitoa kauli hiyo leo(Juni 26) alipokuwa
akizungumza na waandishi wa habari jijini Mbeya kauli inayoonekana kumhusu moja
kwa moja aliyewahi kuwa Waziri mkuu Edward Lowasa ambaye hivi sasa anaonekana
kukimbilia makanisani kwa kuchangia harambee mbalimbali.
Baadhi ya
wachambuzi wa mambo hususani ya kisiasa wamekuwa wakiitaja njia anayoitumia
Lowasa kuwa njia ya kujisafisha na kujitengenezea nafasi nzuri katika uchaguzi
mkuu wa mwaka 2015.
Lakini Nape
amesema wanaccm wanapaswa wautumie uchaguzi wa chama chao mwaka huu kuhakikisha
viongozi wanaomwaga pesa nyingi kwa kutoa misaada wakidhani ni njia nzuri ya
kuwashika wapiga kura wanatupwa nje ili kukisafisha chama chao.
Amesema
kinachopaswa kufanywa na wanachama ni kuhakikisha wanachagua viongozi walio na
uzalendo na chama chao na pia walio na uwezo wa uongozi ili kukijenga chama
hicho badala ya kuwapa uongozi watu wanaonyooshewa vidole kila siku na
wananchi.
Amewataka vijana
hususani walio na elimu kujitosa kupigania uongozi wa chama hicho akisema hatua
hiyo itakiwezesha kupata damu change na zilizo na nguvu ya kukiendeleza badala
ya kukidumaza.
Nnauye amekanusha
pia kauli za baadhi ya watu wanaokejeli dhana ya Kujivua Gamba wakisema
haijafanikiwa kauli aliyosema si kweli kwani dhana hiyo ilibeba mambo mengi
ndani yake.
Amesema dhana hiyo
ililenga kubadilisura ya chama kwa kuongeza damu change hali inayofanyika hivi
sasa ambapo chama kimeanzisha mchakato wa kuwa nam mkoa maalumu kwaajili ya
wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu.
Amesema pia
kuwawajibisha baadhi ya viongozi wasio na sifa tayari mikakati mbalimbali imefanywa
na wapo baadhi ya watu walioachia ngazi mbalimbali pamoja na kuivunja kamati
kuu iliyokuwa chini ya Yusuf Makamba.
“Kuna watu
wamejivua uanachama mpaka ubunge tumeona leo hii mtu anasema dhana ya Kujivua
Gamba haijafanikiwa mi nadhani ni uongo.Lakini pia baada ya chama kutoa muda
kwa wahusika wajiwajibishe na hawakufanya hivyo sasa tuna vikao mbalimbali
vinavyoendelea kpitia kamati za maamuzi na maadili.Huko nako tutatoka na
maamuzi mengine” amesema.
Amesema pia katika
uchaguzi mkuu wa chama hicho mwaka huu majina ya wagombea wanaokabiliwa na
kashfa mbalimbali hayatarejeshwa hivyo ni vema wanachama hao wasijaze fomu
kabisa.
No comments:
Post a Comment