Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, June 15, 2012

SERIKALI INATAMBUA UCHAWI

 KUENEZWA kwa dhana kuwa Serikali haitambui uchawi kumeelezwa kusababishia matukio mengi ya wananchi kujichukulia sheri amikononi ya kuwaua watu wanaohisiwa kuwa wachawi pamoja na kuharibu mali zao.

Mmoja wa maofisa wa kituo cha Sheria na Haki za binadamu (LHRC) Leticia Petro ameyasema hayo na kubainisha kuwa katika kipindi cha mwaka jana zaidi ya mauaji 600 yametokea nchini yakihusisha wananchi kujichukulia sheria mikononi kwa kuwatuhumu wenzao uchawi na kuitaja mikoa ya Shinyanga na Mwanza kuwa inaongoza.

Amesema ni dhana potofu kueleza kuwa serikali haiamini uwepo wa uchawi ilikhali tangu mwaka 1928 iliundwa sheria ya Uchawi nchini na mwaka 2002 ikafanyiwa marekebisho.

Kwa upande wao washiriki wa semina ya mafunzo ya Wasaidizi wa sheria iliyofanyika jijini Mbeya walilalamikia baadhi ya viongozi wa serikali na jeshi la polisi katika ngazi za wilaya wakisema wamekuwa wakiwadanganya wananchi kuwa serikali haiamini uchawi badala ya kuwaelimisha taratibu zinazopaswa kufuatwa pale wanapomtuhumu mtu kuwa mchawi.

No comments:

Post a Comment