Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, June 4, 2012

ZAHANATI SABA KUFUNGULIWA MWEZI HUU

HALMASHAURI ya wilaya ya Mbarali imewahakikishia wakazi wilayani hapa kuwa siku chache zijazo  huduma za afya zitapanuliwa kwa zahanati saba na kituo kimoja cha afya kufunguliwa.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri Aswege Kaminyoge ametoa uhakika huo  alipotembelea  na kukagua zahanati hizo na kusema kabla ya kumalizika kwa mwezi juni zitakuwa zimeanza kutoa huduma.

Kaminyoge amesema kufunguliwa kwa zahanati na kituo kimoja cha afya licha ya kusaidia wagonjwa wengine,kutanusuru afya za akina mama wajawazito ambao kwa sasa wanakabiliwa na adha ya kujifungulia majumbani mwao.

Kwa upande wake Mganga mkuu wa  wilaya hiyo,Dkt. Boniface Kasululu
amekiri  kuanza kufanya kazi kwa zahanati saba na kituo kimoja cha afya kutapunguza kwa kiasi kikubwa vifo vya akinamama wajawazito na watoto vilivyokuwa vikitokana na kutopatikana kwa huduma za wataalamu mara wanapojifungulia majumbani ama njiani wanapotembea umbali mrefu kuja hospitali ya wilaya.

Wakizungumzia adha waliyokuwa wakiipata wakazi wa Kijiji cha Mlungu Jamila Kalinde na Wilison Mbedule walisema wakazi wa kijiji hicho na vingine vya jirani wamekuwa wakitembea umbali wa zaidi ya kilometa 40 kufuata huduma ya afya katika Kituo cha afya cha Kwatwanga, kilichopo katika mkoni Iringa.

No comments:

Post a Comment