Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, June 15, 2012

WANAFUNZI WAPANDA KIZIMBANI

WANAFUNZI 24 wa shule ya sekondari ya seminari ya Manow ya wilayani Rungwe mkoani Mbeya leo(Juni 15) walifikishwa mahakamani kusomewa shitaka la kufanya vurugu zilizopelekea uharibifu mkubwa wa mali za shule zenye thamani ya zaidi ya shilingi 50 milioni.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya mkuu wa wilaya Chrispin Meela amethibitisha wanafunzi hao kufikishwa mahakamani alipozungumza na RFAjijini Mbeya ikiwa ni siku moja tangu tukio hilo litokee.

Meela amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia juni 14 baada ya uongozi wa shule kuwataarifu wanafunzi kuwa kwa usiku huo watalazimika kula chakula kingine badala ya wali kutokana na mchele uliokuwepo kuisha huku mwingine ukiwa haujafikishwa shuleni hapo.

Amesema baada ya kuambiwa hayo wanafunzi hao waliwaongoza wenzao kufanya vurugu kwa kuharibu mali mbalimbali ikiwemo kuvunja milango na madirisha ya majengo mablimbali yakiwamo madarasa.

Mkuu huyo wa wilaya tayari amekwisha ifunga shule hiyo hiyo hadi tarehe Julai 7 mwaka huu wanafunzi watakaporudi tena na kuwataka wale wa kidato cha pili, tatu, Nne na sita kwa kuwa imeonekana kuwa ndio viongozi wa uharibifu huo wajapo shuleni hapo waje na wazazi wao na maelezo binafsi kwa barua.

No comments:

Post a Comment