WAANDISHI WA HABARI WANAOTUHUMIWA KUPOKEA RUSHWA WAFIKISHWA MAHAKAMANI JIJINI ARUSHA
HALI ILIVYOKUWA MAHAKAMANI HAPO WAKATI WA KESI YA WAANDISHI HAO
MMOJA WA WATUHUMIWA HAO AKIWASILI MAHAKAMANI
Na Idd Uwesu- Arusha yetu
Wafanyakazi
watatu wa kampuni ya new habari cooparation waliokamatwa na askari wa
kikosi cha kuzuia na kupamaba na rushwa nchini takukuru kwa madai ya
kuomba na kupokea rushwa ya shilingi laki mbili kati ya milioni moja na
laki nane wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa arusha
kujibu tuhuma zinazowakabili
Watuhumiwa
hao wamesomewa mashataka yao mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa
wa arusha,Yohana Myombo,na mwendesha mashitaka wa taasisi ya kuzuia na
kupamabana na rushwa Hamidu Simbano amedai kuwa watuhumiwa hao
wanakabiliwa na mashitaka mawili ikiwemo kushawishi na kudai rushwa.
Katika
eneo la mahakama ya hakimu mkazi mkoa arusha watuhumiwa hao
waliwasili,huku kando waandishi wa habari pamoja na ndugu jamaa wakiwa
wamefika katika eneo hilo kwa shauku ya kufahamu nini kitajiri katika
kesi hiyo.
Mwendesha
mashitaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU mkoa wa
arusha,Hamidu Simbano ameiambia mahakama kuwa watuhumiwa hao watatu
wanadaiwa kumshawishi mtumishi wa Shirika la Umeme TANESCO wilaya ya
Monduli kutoa rushwa kwa madai ya kutokidhi vigezo vya ajira yake.
Washitakiwa
hao watatu wote wanashitakiwa kwa kosa moja la kushawishi na kudai
rushwa ya shilingi milioni 1.5, ambapo mshitakiwa wa tatu, Mwita Chomete
yeye anadaiwa kuwa mnamo majira ya saa 10 jioni katika wilaya ya
Monduli alipokea shilingi laki mbili kwa niaba ya Masyaga Matinyi.
Washitakiwa wote walikana mashitaka hayo na wako nje kwa dhamana ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi juni 29 mwaka huu.
HABARI NA PICHA NI KWA HISANI YA MTANDAO WA www.arushayetu.blogspot.com
No comments:
Post a Comment