TIMU ya mkoa wa Mbeya kwa mashindano ya
shule za sekondari(Umisseta) alhamisi hii imeondoka kuelekea mkoani Rukwa
tayari kwa kushiriki ngazi ya kanda ya ndanya za juu kusini ya michuano hiyo
itakayoanza Ijumaa ya wiki hii.
Timu hiyo imeondoka ikiwa na jumla ya
wachezaji 140 wa michezo mbalimbali na kati yao wakiwemo Wasichana 71 na
wavulana 69 waliopatikana kupitia mashindano hayo ngazi ya mkoa.
Meneja wa timu hiyo George Mbijima
ambaye pia ni afisa michezo,vijana na utamaduni mkoa wa Mbeya amesema pamoja
naye timu imeongozana na viongozi wengine 11 wakiwamo walimu wa michezo
husika,Mwenyekiti wa timu Juma Kaponda, na mratibu Kasekenya Michael.
Mbijima amewahakikishia wakazi wa mkoa
wa Mbeya kuwa upo uwezekano mkubwa wa timu hiyo kurejesha historia ya ushindi
wa mwaka jana kutokana na maandalizi mazuri iliyofanya wakati ikiwa kambini
kujiandaa.
No comments:
Post a Comment