Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, June 11, 2012

MRADI MKUBWA WA MAJI WAJA MBEYA

HATIMAYE matumaini ya mradi mkubwa wa ujenzi wa miundombinu ya maji ya bomba katika kata ya Itagano Jijini Mbeya unaofadhiriwa na Benki ya Dunia (WB)  kwa mkopo yameanza kuonesha dalili baada ya halmashauri ya jiji kuukabidhi kwa mkandarasi kwa ajili ya kuanza kutekelezwa.

Meya wa jiji la Mbeya Athanas Kapunga leo (Juni 11) ameiwakilisha halmashauri  wakati wa kutiliana saini ya mkataba wa utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo na kampuni ya Geotech ya Jijini Mbeya.

Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Seko Nkusa,mradi huo utajengwa kwa gharama ya shilingi milioni 293,553,571.21  na utekelezaji wake unaanza mara moja baada ya kusainiwa kwa mkataba na ni wa muda wa miezi sita.

Nkusa amesema ujenzi wa mradi huo utasimamiwa na mhandisi mshauri, kampuni ya COWI ya Jijini Dar es Salaam kwa gharama ya shilingi milioni 29.196.

Kwa upande wake meya Kapunga ameishukuru Serikali kwa kusaidia upatikanaji wa mfadhili huyo aliyekubali kutoa fedha za ujenzi wa mradi huo huku akisema hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2010.

Naye  diwani wa Kata hiyo Abel Mbwiga Ndalama amesema kuwa ujio wa mradi huo ni ukombozi kwa wananchi wa kata yake ambao hivi sasa wanatumia maji ya visima vyenye maji ambayo siyo safi wala salama.

No comments:

Post a Comment