Dogo Janja akiwaaga washikaji.
Dogo Janja akiagana na kaka yake mwenye t-shirt ya bluu yenye mistari.
Akiingia ndani ya basi.
Akiwa ndani ya basi.
Safari ya kuelekea AR.
Tiketi ya Dogo Janja.
Jana kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM Msanii
Madee wa Tip Top Connection ambae ndio alikabidhiwa na wazazi kumlea na
kumsimamia Dogo Janja aliamplfy kuhusu sababu za kumrudisha Dogo Janja
mikononi mwa wazazi wake baada ya kudai kumshindwa.
Madee kasema “Dogo Janja aliyekuwa Form
II, Makongo High School kakataa kusoma kwa hiyo mimi siwezi kukaa nae
wakati hataki kusoma, nilikuwa safarini Iringa na Mbeya ambapo baada ya
kurudi mwalimu wake wa darasa alinipigia simu na kunipa pole kwa sababu
Dogo Janja anaumwa, nikashtuka ikabidi nimpigie nikawa simpati kwenye
simu, nikaenda nyumbani kwa Tunda Man alipokuwepo na alipojua nimekuja
akajificha alikuwa anataka kunikimbia nikampiga sana vibao, kweli
nilimpiga ambapo kesho yake baada ya kuamka nikamuuliza unataka kusoma
au kuzurura mtaani? akajibu kwamba anataka kwenda kusoma Arusha ikabidi
nimpigie baba yake palepale ambapo mzee wake alniomba nisimrudishe
Arusha niendelee kukaa nae”
Madee ameendelea kusema kwamba
“nilimwacha nyumbani baada ya kuchukua simu yake ambapo nilikuta vitu
vingi sana vya kishenzi shenzi kaviandika na ninavyo mpaka leo kwa ajili
ya ushahidi, vimeniumiza hasa kwa mtu kama mimi ambae najua nimemtoa
wapi, kaandika kuhusu uchafu mbaya na kingine kinanihusu mimi ambacho
hapaswi kusema kwa mtu kama yeye, baada ya hapo msimamo wake ulikuwa
vilevile kwamba anataka kurudi kwenda kusoma Arusha, jioni tukakaa kikao
(juzi) na kaka yake na watu wengine na mimi nikampa baraka zote”
Kwenye sentensi nyingine Madee amesema
“kwa wiki iliyopita na wiki hii Dogo Janja alitoroka kwenda shule kwa
siku tatu na hii ni mara ya pili ambapo mara ya kwanza nilimpeleka shule
na kumchapa mbele ya wanafunzi wenzake, yaani nilivyompeleka shule
wanafunzi wenzake mpaka walikuwa wanamshangaa, alisingizia vitu vingi
vya uongo alikuwa ananidanganya mimi nyumbani na siku hiyo ndio
nilimkuta Ubungo Plaza alikuwa anaogelea na rafiki yake, walimu wake
waliniambia hawajamuona shule kwa muda wa wiki moja”
No comments:
Post a Comment