Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, April 21, 2015

MBUNGE,MWENYEKITI CCM NUSURA WAZICHAPE KAVU KAVU MBELE YA WAZIRI

 Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu(Kushoto) na Mbunge wa Mbarali Dickson Kilufi wakisaini vitabu vya wageni baada ya kuwasili Ubaruku kuwasikiliza wananchi juu ya mgogoro wa mpaka kati ya vijiji 21 na Tanapa.

 Moja ya mabango yaliyoandikwa ujumbe na wananchi wahanga wa uhamisho
 Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu wakiwa na
Mwenyekiti wa CCM wilaya Mathayo Mwangomo baada ya kuhutubia wananchi.





                                 HABARI KAMILI

KATIKA kuonesha hali si shwari ndani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) wilayani Mbarali,mbunge wa jimbo hilo Mbarali Dickson Kilufi na Mwenyekiti wa CCM wilaya Mathayo Mwangomo,hivi karibuni nusura wapigane Mbelea ya waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu.

Nyalandu aliwasili wilayani humo majira ya jioni kwajili ya kufuatilia mgogoro wa kimpaka wa ardhi kati ya Tanapa na wakazi wa vijiji vilivyopo jirani na hifadhi ya taifa ya Ruaha katika eneo la Ihefu.

Baada ya kufika wilayani hapa ilikiwa Nyalandu akutane kwanza na wajumbe wa kamati ya Siasa ya wilaya ya Chama Cha Mapinduzi ili kupata maoni yao kabla ya kukutana na uongozi wa serikali wilaya na kisha wananchi katika kata ya Ubaruku.

Lakini kutokana na waziri kufika kwa kuchelewa alilazimika kushauriana na viongozi wa chama kuahirisha vikao hivyo na badala yake vifanyike kesho yake ili kutoa fursa kwa makundi yote kushirika katika utatuzi wa mgogoro uliodumu kwa takribani miaka saba sasa.

Hata hivyo mbele ya kiongozi huyo,Mbunge Kirufi na mwenyekiti wake wa Chama walishindwa kuficha utofauti walionao na badala yake walianza kurushiana maneno makali(matusi) mbele yake huku kila mmoja akionesha kuwa mbabe zaidi ya mwenzie.

Chanzo cha habari cha uhakika kilichokuwepo eneo la tukio kilieleza kuwa viongozi hao waliendelea kurushiana matusi hadi pale Nyalandu alipoamua kuingilia kati kuwasuluhisha na baadaye yeye kuamua kwenda jijini Mbeya kupumzika kabla ya kurejea wilayani hapa kesho yake.

Uthibitisho wa tukio hilo ulibainika katika ukumbi wa CCM wilaya,wakati Nyarando alipowataka wawili hao wapeane mkono kuashiria hali ya jana yake imekwisha mbele ya wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya huku pia akiwasisitiza viongozi hao kuwa na umoja katika kupigania maslahi ya chama na wananchi wanaowaongoza.

Hata hivyo Mbunge Kilufi katika kuonesha kuwa bifu halijakwisha licha ya kukubali kupeana mikono ukumbini,alipopanda jukwaani mbele ya wananchi wa kata ya Ubaruku alionesha kuendelea kuwa na kinyongo mbelea ya baadhi ya viongozi wa CCM wilaya japok hakuwataja majina.

“Hata kama unamchukia Kilufi,endelea kumchukia,lakini katika suala la mpaka kati ya Tanapa na wananchi naomba tuungane kuwatetea watu wetu” yalikuwa maneno ya Kilufi jukwaani.

Baadhi ya wakazi wilayani hapa wanasema ugomvi baina ya wawili hao unatokana na kuwa ufuasi katika makundi mawili tofauti ya watu wanaowania nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu ujao ambao mbunge anatajwa kuwa katika kundi la waziri wa zamani Edward Lowasa.

Lakini wapo pia wanaosema mwenyekiti wa chama wilaya amekuwa akipingana na mbunge huyo katika suala la mpaka kati ya Tanapa na vijiji vya jirani kwa kile wanachoeleza kuwa amekula rushwa kutoka Tanapa tuhuma alizozitaja pia mwenyekiti huyo alipozungumzia suala la mpaka akiwa ukumbini.

“Mh.waziri suala hili la mpaka wengine hata limetupaka matope,wapo wanaosema tumeingizwa mifukoni mwa Tanapa.Wanasema Tanapa wametununua kwa kutupa fedha ili tusiwatetee wananchi.Tunaomba tulipatie ufumbuzi ili mambo haya yasiendelee” alisema Mwangomo alipokuwa ukumbini.

No comments:

Post a Comment