Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, April 1, 2015

NANI MSALITI WA KIJANA WA KITANZANIA?














 Hawa ndiyo waliobinafsishiwa kiwanda na sasa hakifanyi kazi.Majengo yamegeuka mradi wa maghala kupangishia kampuni nyingine.




KILIO kikubwa kwa vijana wa kitanzania ni ukosefu wa ajira kwa kundi hilo muhimu.Moja ya mambo yanayokwamisha upatikanaji wa ajira katika maeneo mbalimbali ni pamoja na sera mbovu ya ubinafsishaji wa  makampuni na viwanda vya umma uliofanyika miaka kadhaa iliyopita.

Ubinafsishaji huu ambao haukuzingatia maslahi ya watanzania walio wengi,ulifanyika huku watawala wakijua watu wanaobinafsishiwa hawana uwezo wa kuendesha Makampuni ama viwanda wanavyobinafsishiwa.

Kiwanda cha Zana Za Kilimo maarufu kama ZZK ni moja kati ya viwanda vilivyokuwa vikizalisha ajira kwa wingi na kutoa ukombozi wa kiuchumi kwa vijana wa mkoa wa Mbeya na mikoa ya jirani.Lakini kiwanda hiki kama ilivyo kwa vingine kilibinafsishwa kwa mtu asiye na uwezo wa kukiendesha.

Hivi sasa mmiliki wa kiwanda hiki ambacho mashine na vipuri vinaendelea kuozea ndani ya majengo huku pia vikiwa vimegeuka makazi ya mijusi na nyoka wenye uwezo wa kuishi maeneo ya baridi hakiendeshi.Badala yake amegeuka baba mwenye nyumba na kuanza kupangisha majengo ya kiwanda hiki kwa makampuni mengine.

Moja kati ya kampuni zilizopanga mahali hapa ni kampuni ya SBL ambayo inatumia sehemu ya majengo ya kiwanda hiki kama maghala ya kuhifadhia bidhaa zake yaani bia.

Lakini wakati watanzania hususani vijana wa mkoani Mbeya wakilalamikia kufungwa kwa kiwanda hiki,vijana wachache wanaonekana wasaliti kiasi cha kufurahia hata uzinduzi wa ghala hili kama unavyowaona kwenye picha mbalimbali za hapo juu wakicheza baada ya kupewa bia za bureeeeee.

Viongozi nao walishiriki kwenye uzinduzi wa ghala hili kama unavyowaona wachache kwenye hizo picha.Wapo viongozi waliostuka na kukacha ufunguzi huo,lakini kwa kuogopa lawama za mabosi wa kampuni hii wakawatuma wawakilishi.

Sote tujiulize,hivi mwekezaji huyu alipewa kiwanda ili azalishe zana za kilimo au kupangisha majengo kwa makampuni mengine.Na je kama vijana wa kitanzania hawawezi kuwa na msimamo kiasi cha baadhi kufurahia wakati wengine wanalia ni lini kilio chao kitasikilizwa?

No comments:

Post a Comment