Na Mwandishi wetu, Dodoma
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ametoa kiasi cha Shingi Milioni mbili kwa timu ya Mbeya City ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya timu hiyo kuelekea mchezo dhidi ya Kagera Sugar.
Akikabidhi zawadi hiyo kwa niaba ya Mhe. Spika wa Bunge, Mbunge wa Jimbo la Lupa Chunya kwa kushirikiana na wabunge wa Mbeya nao wametoa kiasi cha Shilingi milioni moja kama sehemu ya motisha kwa wachezaji
Kiasi kilichotolewa na Spika pamoja na wabunge wa Mbeya kinafikisha jumla ya Shilingi milioni tatu.
Pamoja na mambo mengine, Wabunge hao wameahidi kununua ushindi kwa timu ya Mbeya City kwa kila mechi zilizosalia kwenye ligi Kuu ya Tanzania inayoendelea.
No comments:
Post a Comment