WANAFUNZI wa Kike mashuleni wametakiwa kuepukana na
Ahadi za kuonana baadaye kwakuwa kufanya hivyo kunaweza pia kuwasababishi kushindwa
kufikia malengo yao ya baadaye.
Mkuu wa mkoa
wa Mbeya,Amos Makalla alipiga marufuku ahadi hizo aliupokuwa akizungumza na
wanafunzi wa Shule ya Sekondari Madibira iliyopo katika kata ya Madibira
wilayani Mbarali.
Makalla alisema kuna tabia iliyojengeka kwa
wanafunzi wa vidato vya juu kuwarubuni waliopo vidato vya chini na kuwashawishi
kuanzisha mahusiano ya kimapenzi kwa madai kuwa watawaoa baada ya kumaliza
shule.
“Wapo wanafunzi wa kiume ambao kwa kuwa wapo kidato
cha nne au cha sita wanaanza kuwadanganya mabinti walioko vidato vya
chini..Ooooh unajua mimi ntatangulia kumaliza shule…kwahiyo usijali utakuta
mimi nimeshakuandalia maisha hivyo nitakuoa.Hakuna kitu kama hicho na kuanzia
leo usikubali ahadi ya namna hiyo”
“Muhimu ni kuzingatika kilichokuleta hapa
shuleni.Malengo yako ya kuwa hapa ni nini? Haukuja kutafuta mchumba hapa
ulikuja kusoma ili baadaye ufikie malengo yako. Hapa tuna wanasiasa na
wataalamu mbalimbali sasa usikubali ndoto yako kufutika kwa ahadi ya
kukuoa”alisisitiza Makalla.
Mkuu huyo wa mkoa pia alitoa muda wa wiki mbili kwa
Halmashauri ya wilaya ya Mbarali na Tanesco
kuhakikisha wanatatua changamoto ya kutopatikana kwa maji shuleni hapo
kutokana na kutokana na kutofungwa kwa mashine ya kusukuma maji.
Alisema kutopatikana kwa maji safi na salama shuleni
hapo kunahatarisha afya ya wanafunzi na walimu na pia kunasababisha changamoto
ya kutumia muda mwingi kuyafuata maeneo ya mbali.
No comments:
Post a Comment