Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, February 16, 2018

RC MAKALLA APOKEA MSAADA WA VYUMBA VYA MADARASA

 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Amos Makalla akikata utepe kuashiria kupokea vyumba viwili vya madarasa na kimoja cha Ofisi ya walimu vilivyojengwa kwa msaada mkubwa wa Kampuni inayojishughulisha na unuzuzi wa zao la Kakao wilayani Kyela ya Kim’s chocolate(Belgium) Bioland International katika Shule ya msingi Ngana wilayani hapo.Wengine ni maafisa kutoka kampuni hiyo na Mkuu wa wilaya ya Kyela Claudia Kita.


Wanafunzi wa Shule ya Msingi Ngana wikicheza kwenye hafla ya kupokea vyumba vya madarasa shuleni kwao.





MKUU wa Mkoa wa Mbeya,Amos Makalla amepokea vyumba viwili vya madarasa na kimoja cha Ofisi ya walimu vilivyojengwa kwa msaada mkubwa wa Kampuni inayojishughulisha na unuzuzi wa zao la Kakao wilayani Kyela ya Kim’s chocolate(Belgium) Bioland International katika Shele ya msingi Ngana iliyopo wilayani humo.

Makalla pia amepokea madarasa vyumba viwili vya madarasa vilivyojengwa na Kampuni hiyo katika Shule ya Msingi Lubele iliyopo katika kata ya Ikimba.

Kwa mujibu wa Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela,Mwalimu Polemone Ndarugiliye ujenzi wa vyumba vitatu katika shule ya msingi Ngana ulioambatana na ukarabati wa vyumba vingine viwili shuleni hapo uligharimu Shilingi 23,271,000 ambapo kampuni ya Bioland ilichangia Shilingi 17,000,000 sawa na asilimia 73.1,wananchi Shilingi 5,128,000 sawa na asilimia 22 kupitia nguvu kazi.

Mwalimu Ndarugiliye alisema Serikali kupitia fedha za mfuko wa jimbo ilichangia shilingi 600,000 sawa na asilimia 2.6 na Shule ya Msingi Ngana kupitia fedha za ruzuku ikachangia Shilingi 534,000 sawa na asilimia 2.3.

Alisema kwa Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya msingi Lubele uliogharimu Jumla ya Shilingi 14,756,500 mchango wa Kampuni hiyo ni Shilingi 9,821,000,wananchi kupitia nguvu kazi Shilingi 4,352,000,Diwani Shilingi 682,000 na madhehebu  mbalimbali ya dini Shilingi 201,000.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo,Makalla aliwataka wakazi wilayani hapa kuendelea kushirikiana kwa karibu na Kampuni hiyo kwakuwa inaonyesha jitihada nzuri za kuboresha miundombinu ya Elimu.

“Ukibebwa uwe tayari kutoa ushirikiano.Hawa wanaendelea kutuchangia kwakuwa na ninyi mmekuwa mstari wa mbele kushiriki katika utekelezaji wa miradi inayoanzishwa kwenye maeneo yenu.Lakini pia hili ni fundisho kuwa kama watu wa kutoka mataifa mengine wana utayari wa kuchangia maendeleo ya kumkomboa mtoto wa hapa Kyela kielimu kwa nini wewe mtanzania wa haapa ugome?”

“Lakini ni muhimu pia kutambua kuwa kinachotukutanisha na wadau hawa ni zao la Cocoa.Sasa ni wakati kwetu kutambua kuwa zao hili lina faida hivyo tuhakikishea tunalima zaidi ili siku zijazo hawa washawishike kuja kujenga kiwanda japo cha kuchakata zao hili katika hatua za awali hapa kwetu”alisisitiza Makalla.

Kwa upande wake Afisa kutoka Kampuni ya Bioland,Fons Maex alisema kampuni bado ina utayari wa kuendelea kusaidia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu katika Shule zote za msingi zilizopo kwenye Halmashauri za Kyela,Rungwe na Busokelo.

“Mmeomba majengo mengine hapa Ngana.Nimechungulia leo kwenye kapu langu nimeona bado nina fedha za kutosha.Tutajenga hapa jengo litakalokuwa na vyumba viwili vya madarasa na pia maktaba na stoo.Kama mko tayari tuanze kesho ujenzi.Lakini pia shule mpya mnaotaka kuipachua kutoa shule ya msingi Kasumulu tunaahidi tutajenga madarasa nane.Ninyi andaeni utaratibu tu sisi tuanze kazi”alisisitiza Maex.

No comments:

Post a Comment