JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA.
Ofisi ya Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa
Mbeya,
Namba ya simu 2502572
S. L. P. 260,
Fax - +255252503734
MBEYA.
E-mail:- rpc.mbeya@tpf.go.tz
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 05.01.2017.
Mnamo tarehe 04.01.2017 majira ya saa
06:00 asubuhi huko maeneo ya Kitongoji cha Songambele kilichopo Kata ya Ilembo,
Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Kipolisi Mbalizi, Mkoa wa Mbeya, Mtu mmoja
aliyefahamika kwa jina la YELA AMONI
[30] mkazi wa Italazya aliuwawa
baada ya kushambuliwa na wananchi wenye hasira kali kwa mawe na fimbo wakati
akifukuwa kaburi alilozikwa SISTA SISALA
mwenye ulemavu wa ngozi (albino) aliyefariki dunia tarehe 28/02/2010 na kuzikwa tarehe 29/02/2010
kwenye makaburi yao ya familia.
Awali
majira ya saa 00:30 usiku wa kuamkia
tarehe 04.01.2017 marehemu na
wenzake wawili walifika kaburini hapo na kuanza kufukua kaburi lakini kabla
hawajamaliza wananchi waligundua na kuwazingira lakini wawili walikimbia na
kufanikiwa kumkamata JONAS JOHN [28] mkazi wa Chapakazi akiwa ndani ya
kaburi akifukua ambaye kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano.
Kutokana
na hali hiyo, wananchi wa eneo hilo waliendelea kulinda kaburi hilo kwa siri na
ndipo marehemu YELA AMONI alirudi kaburini
hapo na kutaka kuendelea kufukua na ndipo wananchi hao walipomzingira na kuanza
kumshambulia hadi kufariki dunia. Chanzo cha tukio hili ni imani za kishirikina
kwani marehemu na wenzake walikuwa wanataka mifupa ya marehemu SISTA SISALA ambaye alikuwa mlemavu wa
ngozi [albino]. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali Teule Ifisi. Upelelezi
unaendelea.
Mnamo tarehe 05.01.2017 majira ya saa
06:00 asubuhi huko Mikumi, Kata ya Kyela, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya
Kyela, Mkoa wa Mbeya, Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la HILDA SIGARA [30] Mkazi wa Mikumi
alifariki dunia akiwa anapelekwa Hospitali kwa matibabu baada ya kupigwa nyundo
kichwani na mume wake aitwaye REBSON
TWEVE umri kati ya miaka 30 – 35 Mkazi wa Mikumi Wilaya ya Kyela.
Inadaiwa
kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi kwani inasadikiwa mtuhumiwa
alikuwa akimtuhumu marehemu kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mwanaume
mwingine.
Mtuhumiwa
alitoroka mara baada ya tukio na juhudi za kumtafuta zinaendelea. Eneo la tukio
kumekutwa nyundo moja, kisu kimoja na fimbo ya muanzi ambavyo vinasadikiwa
kutumika katika tukio hilo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya
Kyela ukisubiri kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu. Upelelezi unaendelea.
Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya
limeendelea kukabiliana na matukio makubwa ya uhalifu pamoja na wahalifu. Jitihada
zinaendelea kwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha Mkoa wetu unakuwa mahala
salama. Hata hivyo kumekuwa na taarifa ya vifo na kujinyonga kama ifuatavyo:-
TAARIFA ZA VIFO:
Mnamo tarehe 05.01.2017 majira ya saa
06:30 asubuhi huko maeneo ya Majengo, Kata ya Nonde, Tarafa ya Sisimba,
Jiji na Mkoa wa Mbeya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilipokea taarifa kuwa Mtu
mmoja aliyefahamika kwa jina la EDWARD
PETER [60] Mfanyabiashara na Mkazi wa Majengo amekutwa amefariki dunia
chumbani kwake.
Mwili
wa marehemu haukukutwa na jeraha lolote. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika
Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa uchunguzi zaidi wa kitabibu. Upelelezi unaendelea.
Mnamo tarehe 04.01.2017 majira ya saa
15:00 alasiri Kijiji cha Kiwanja, Kata ya Mbugani, Tarafa ya Kiwanja,
Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya, Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la ABIUDI COSMAS [18] Mkazi wa Kiwanja
Wilayani Chunya alifariki dunia baada ya kuangukiwa Kifusi cha Mchanga wakati
anajaribu kuchimba madini ya dhahabu.
Mwili
wa marehemu umefanyiwa uchunguzi wa kitabibu na kukabidhiwa ndugu kwa mazishi.
TAARIFA YA KUJINYONGA:
Mnamo tarehe 05.01.2017 majira ya saa
00:20 usiku huko Kijiji na Kata ya Mbugani, Tarafa ya Kiwanja, Wilaya ya
Chunya, Mkoa wa Mbeya, Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la ROBERT MWAISENYE [18] Mkazi wa Mbugani alikutwa amefariki dunia
baada ya kujinyonga kwa kutumia kamba ya manila akiwa ndani ya nyumba yake.
Chanzo
cha tukio hili bado hakifahamika, uchunguzi zaidi unaendelea kufanyika ili
kubaini chanzo chake. Upelelezi unaendelea.
WITO:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishna wa
Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI anatoa
wito kwa jamii kuacha tamaa mali/fedha kupitia njia zisizo halali kwani Jeshi
la Polisi halitaruhusu wala kufumbia macho vitendo kama hivyo na badala yake
wajishughulishe na kazi halali kwa lengo la kujipatia kipato halali kuendesha
maisha yao. Aidha Kamanda KIDAVASHARI anaendelea kutoa wito kwa
wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani ni kosa kisheria na badala
yake wawafikishe kwenye mamlaka husika watuhumiwa wanaowakamata kwa tuhuma
mbalimbali kwa hatua zaidi za kisheria.
Imesainiwana:
[DHAHIRI A.
KIDAVASHARI - DCP]
KAMANDA
WA POLISI MKOA WA MBEYA.
No comments:
Post a Comment