Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, August 2, 2012

MWAKALEBELA NA MUNGAI WASAKWA NA TAKUKURU IRINGA

Siku Mwakalebela na mkewe walipopandishwa kizimbani na TAKUKURU Iringa
Siku Mungai alipopandishwa kizimbani na TAKUKURU Iringa

TAASISI ya kuzuaia na kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Iringa yazidi kumng’ang’ania aliyekuwa waziri wa wizara mbali mbali katika awamu mbali mblia katika serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Mufindi Kaskazin Joseph Mungai kwa lengo la kumfikisha mahakamani ili kujibu mashitaka ya kujihusisha na rushwa katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM mwaka 2010.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mjini Iringa kaimu mkuu wa Takukuru mkoani hapa Stephen Mafipa amesema taasisi hiyo inamtafuta mheshimiwa mungai ili kumfikisha mahakamani kujibu mashitaka hayo baada ya mahakama kuu kanda ya Iringa kupitia kwa jaji kiongozi wa mahakama hiyo sekieti kihio kutupilia mbali rufaa yake.

katika rufaa yake aliyokata kupitia kwa mawakili wake wawili basiri mkwata na Alex Mgongolwa Mungai aliiomba mahama hiyo kutupilia mbali uamuzi wa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Iringa kupitia kwa mheshimiwa marry senapee tarehe 31 january 2011 ambapo alitupilia mbali hati yamashitaka ya rushwa yaliyokuwayakimkabli mheshimiwa mungai na kuamuru upande wa mashitaka kufanyia marekebisho hati hiyo na kumfikisha mahakamani mtuhumiwa.

katika rufaa yake mh.mungai aliiomba mahakama hiyo kutupilia mbali uamuzi wa mahakama ya hakimu mkazi na kisha kutolea maamuzi hoja nyingine ambazo hazikutolewa maamuzi na mahakama hiyo ya hakimu mkazi ambapo katika makosa yote 15 ya kutoa rushwa ambayo mungai alikuwa akishitakiwa nayo yalikuwa siyo makosa ya jinai kwa kukosa maneno muhimu kisheria kama inavyotakiwa katika kifungu cha 15 (1)(b) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.

katika hoja ya pili bwana mafipa amefafanua kuwa kifungu cha 21(1) (a) na kifungu cha 24 (8) cha sheria ya gharama za uchaguzi,sheria namba 6 ya mwaka 2010.ambacho mheshimiwa mungai na wenzake walishitakiwa nacho kilikuwa hakitengenezi kosa la jinai kisheria .

Aidha taasisi hiyo inakusudia kumkamata na kumfikisha mahakamani aliyekuwa katibu mkuu wa chama cha soka nchiniTFF Fredrick Mwakalebela ili kujibu kesi kama hiyo ya rushwa ya uchaguzi mwaka 2010 baada ya rufaa yake inayofanana na ya mheshimiwa mungai kutupiliwambali na mahakama kuu kanda ya Iringa siku chache zilizopita.

Mungai na mwakalebela walikuwa wagombea ubunge katika majimbo ya mufindi kaskazini na Iringa mjini ambapo wote wanatuhumiwa kuwa walitumia ushawishi wa rushwa kwa wapiga kura katika mchakato wa kura za maoni ndani ya chama cha mapinduzi ccm.

No comments:

Post a Comment