WATU
watano wamefariki dunia mkoani Mbeya katika matukio matatu tofauti likiwemo la
familia ya mama na watoto wake wawili waliofariki kufuatia ajali ya moto ulioteketeza
nyumba yao wakiwa wamelala.
Kwa
mujibu wa kaimu kamanda wa polisi mkoani Mbeya
mrakibu mwandamizi Barakiel Masaki, tukio hilo lilitokea Agosti 16 mwaka huu majira ya saa 4:55 usiku.
Alisema
wanafamilia hao wakiwa wamelala nyumba yao ilianza kuwaka moto na kwamba
walipoteza maisha kutokana na kukosa hewa kufuatia moshi mzito ulioenea ndani
ya nyumba.
Amewataja wanafamilia hao waliokufa ni
mama mzazi Upendo Paul(24) na watoto wake
ambao ni Tecra Paul (4) na Aman Paul wote wakazi wa Ilemi darajani jijini Mbeya.
Masaki
alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo mpaka sasa bado hakijajulikana na miili ya
maremu hao imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa mkoani hapa.
Aidha ametoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari kutokana na
majanga ya moto yanayotokea mkoani
hapa.
Wakati
huo huo mkazi wa majengo Mkwajuni
wilayani Chunya Sprian
Majiyashamba(58) anashikiliwa na jeshi la polisi baada ya kuumua mke wake kwa
kumchoma kisu kutokana ugomvi wa kifamilia.
Kaimu
kamanda Masaki amesema marehemu alifahamika kwa jina la Secilia Dotabarabara(64) ambaye
alichomwa kisu na mume wake kwenye titi la kushoto na kusababisha kifo
chake papo hapo.
Masaki amesema kuwatukio hilo lilitokea Agosti 16
mwaka 2012 majira ya saa 4:00 katika kijiji cha majengo wilayani chunya na kutaja chanzo cha kifo
hicho kuwa ni ugomvi wa kifamilia.
Katika
tukio lingine mwanamke mmoja mkazi wa kijiji cha nyakazobe wilayani Mbarali amemuua mume wake
kwa kumpiga na kitu kitu kizito kichwani
kutokana kutokana na na ugomvi wa kifamilia.
Akielezea
tukio hili Masaki amesema limetokea Agosti 16 mwaka
huu majira ya saa 3:00 usiku kijijini hapo,na kwamba Christina Msiyunga(24)
alimuua mume wake Geoge Lova(26) kwa kumpiga na kitu kizito kichwani na
kusababisha kifo chake papo hapo.
Amesema mtuhumiwa
wa tukio hilio amekamtwa na atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi
kukamilika,aidha aliwaomba wananchi
kutatua migogoro kwa amani ili kuepukana na vifo visivyo vya lazima.
No comments:
Post a Comment