Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, February 13, 2015

MFUMO DUME WASABABISHA WATOTO KUZIDI KUFANYIWA UKATILI



 Mwanahabari Fredy Jackson akichangia maoni katika warsha ya mafunzo ya uandishi wa habari za Ukimwi na Ukatili wa kijinsia na wa watoto iliyofanyika mkoani Mbeya
 Wanahabari wakipitia nakala ya gazeti la habarileo kuona iwapo lina japo habari moja inayohusu ugongwa wa Ukimwi walipokuwa kwenye makundi kwenye wa warsha ya siku tatu ya mafunzo ya uandishi wa habari za Ukimwi,ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto yaliyoandaliwa na ofisi ya mratibu wa Ukimwi mkoa wa Mbeya kwa ufadhili wa shirika la kuhudumia watoto duniani(Unicef).
Mwanahabari mkongwe Charles Kayoka akifafanua jambo kwa waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo ya uandishi wa habari za Ukimwi na ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto

                              HABARI KAMILI
 KUENDELEA kwa mfumo dume katika jamii kumeonekana kuzidi kuendeleza ukatili dhidi ya watoto wanaozaliwa nje ya ndoa kutokana na mama zao kuficha ukweli kwa kutowaeleza waume zao kuwa si baba wa watoto hao.

Kwa mujibu wa sheria ya mtoto ya mwaka 1971 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,miongoni mwa haki alizonazo mtoto ni pamoja na kuwafahamu wazazi wote wawili na ndugu zao.

Lakini katika jamii baadhi ya watoto wameendelea kufichwa baba zao halisi kutokana na wanawake kutokuwa na nguvu ya kubainisha ukweli juu ya watoto hao kwa waume wanaoishi nao tofauti na ilivyo kwa wanaume wanaozaa nje ya ndoa.

Hali hiyo ilibainika pale wanahabari mkoani Mbeya waliopo kwenye mafunzo ya Uandishi wa habari za VVU/Ukimwi na Ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto walipozungumza na baadhi ya wakazi katika mji wa Mbalizi wilayani Mbeya.

Wakizungumza katika maeneo tofauti mjini hapo baadhi ya wakazi hao walisema wanawake wanaozaa watoto wao nje ya ndoa zao hawana uwezo wa kuwatambulisha watoto hao kutokana na hofu ya kuvunja ndoa zao pale inapobainika tofauti na ilivyo kwa wanaume.

Baadhi ya wakazi Joyce Mwile,Vanesa Muhada na Shayo Katina walisema kutokana na mfumo dume habari zimekuwa zikizagaa katika jamii juu ya uwepo wa wanawake walio ndani ya ndoa kuzaa nje ya ndoa zao lakini wanawake hao hawaweki wazi masuala hayo kwa waume zao.

“Wanaume wanaweza na wamekuwa wakifanya hivyo mara nyingi.Hii inatokana na mfumo wa kimaisha tangu kuumbwa kwa dunia hii.Na kama ni haki ya mtoto kuwajua wazazi basi wapo watoto wengi wanaofanyiwa aina hii ya ukatili” alisema Katina.

Hali hii inaonekana kuwa mbaya zaidi pale ambapo viongozi wa dini nao wanashauri kuendelea kutunzwa kwa siri juu ya watoto wanaotokana na mimba zilizotungwa nje ya ndoa kwa madai kuwa kufanya hivyo kutawezesha ndoa kutovunjika.

Mchungaji Erick Kombe wa kanisa la Consuming Fire Centre tawi la Nsalala Mbalizi alisema kuna uwezekano pia wa wanawake kuuawa iwapo watatoa siri kwa waume zao iwapo walichepuka na kuzaa nje ya ndoa

Wajibu wa jamii katika kuwezesha watoto wanaozaliwa nje ya ndoa ni kutafuta namna itakavyowawezesha wanawake nao kuanza kuweka bayana juu ya mimba zinazotungwa nje ya ndoa kama ilivyo kwa wanaume lengo likiwa ni kuwapa watoto haki ya msingi ya kuwatambua wazazi wao.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment