Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, February 17, 2015

WANAFUNZI TUNDUMA WAFUNGA BARABARA KWA MUDA



 Wanafunzi kutoka shule mbalimbali mjini Tunduma Momba wakiwa barabarani kuandamana kwa kutaka serikali kujenga matuta katika barabara ya Mbeya Sumbawanga kutokana na mwanafunzi mwenzao kugongwa na kufa pamoja na wengine kujeruhiwa huku Polisi wakijaribu kuangalia hali ya usalama






 Mkuua wa wilaya ya Momba Abiud Saidea akiwasili eneo la tukio




                           HABARI KAMILI

WANAFUNZI wa shule Mbalimbali za  msingi wilayani katika mji mdogo wa Tunduma wilayani Momba Mkoani Mbeya,wameandamana barabarani wakiishinikiza Serikali  kujenga matuta katika barabara inayo toka Mjini Tunduma hadi   Sumbawanga mkoani Rukwa kutoka na kutokea kwa ajari za mara kwa mara.

 Maandamano ya wanafunzi hao hayo yametokea leo asubuhi majira ya saa 3  ni baada ya Wanafuzi wawili kugongwa papo hapo na kusababisha mmoja kuaga dunia na wawili kuwa majeruhi katika ajari iliyo tokea jana katika maeneo ya Transforma mtaa wa Mwaka wilayani hapa. 


 Wakizungumza maeneo ya mandamano katika  umati wa wanafunzi wa shule hizo, huku wakiimba nyimbo  za kuishinikiza serikali kujenga  matuta eneo hilo ambalo limekuwa likisababisha ajari mara kadhaa.


 Wasema eneo la Transifoma  ni eneo ambalo mara kwa mara limekuwa likisababisha ajari kutokana na kukosekana kwa matuta ya  kuzuia mwendokasi  wa magari bila kujali kuwa ni kivuko cha wanafunzi.


 “Tunaitaka serikali kutujengea matuta eneo hili maana wanafunzi wengi wamepoteza maisha kwa kugongwa na magari ” alisema mwanafunzi aliyejitambulisha kwa jina  la Ally.

 Hata hivyo waliishinikiza seikali kwa kuitaka iharakishe kuchukua hatua hiyo mara moja ili kuepusha majanga hayo. 


 Pia,kwa upande wa Wananchi wamesema kuwa ni haki yao kwa wanafunzi hao kudai haki yao na ukiangalia idadi ya watu waliogongwa  na magari katika eneo hili ni Wakubwa ni watu nane na watoto 10 kitu ambacho kinasadikika ni mwendokasi wa Madereva.

Akizungumza mbele ya umati wa wanafunzi diwani wa kata ya Tunduma Frank Mwakajoka aliitaka serikali  kuanza mara moja ujenzi wa matuta hayo ili kupunguza ajari za wanafunzi na watu wazima maeneo hayo.

“Tunaitaka serikali kuanza leo ujenzi wa matuta eneo la Transfoma maana tumechoka kupoteza maisha ya watu kwa ajari zinazo zuilika” amesema Mwakajoka.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Momba Abiudi Saidea amewata wanafunzi pamoja na wazazi kuwa watulivu wakati serikali ikitekeleza ujenzi wa matuta eneo hilo hatari , lililopoteza maisha ya watu wengi.

 Amesema ujenzi huo utaanza mara moja bila kuchelewa , na aliwahidi kuwa ameshaongea na uongozi wa Tanroad  wa makao makuu ya mkoa wa Mbeya ili waje wapime eneo hilo na kuanza ujenzi wa matuta hayo.

HABARI NA PICHA KWA HISANI YA MITANDAO MBALIMBALI YA KIJAMII

No comments:

Post a Comment