WATU
wawili wamefariki dunia na wengine 18 kujeruhiwa vibaya baada ya kuungua na
moto ulioripuka wakiwa wanajaribu kuiba mafuta aina ya petrol baada ya lori
lililokuwa likisafirisha kupinduka.
Taarifa
iliyotolewa na jeshi la polisi mkoani Mbeya kwa vyombo vya habari zinaeleza
kuwa walipoteza maisha katika ajali hiyo ni pamoja na mwanamke Maria Pajela(18)
na Wiliam Pascal(38),wote wakazi wa kijiji cha Idweli wilayani Rungwe.
Kamanda
wa Polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi kupitia taarifa hiyo alisema tukio hilo lilitokea jana(Feb18) majira ya saa
tatu usiku katika kijiji cha Idweli, kata ya Isongole, Tarafa ya ukukwe wilayani
hapa.
Kamanda
Msangi alisema katika tukio hilo marehemu hao wawili kabla ya vifo vyao wakiwa
na baadhi ya wakazi wengine wa kijiji cha Idweli walikuwa katika harakati za
kuiba mafuta kutoka katika gari aina ya Scania lenye namba za usajili T
891 AQZ likiwa na tela lenye namba T 821 ARF likitokea Dar es salaam kwenda
nchini Malawi.
Amewataja
majeruhi katika ajali hiyo ambao kati yao wanaume ni 13 na wanawake watano kuwa
ni pamoja na Shukuru Kanzale (21),Nuru George (30), Asante Boniface(38), Joseph
Jamson (18), Joseph Paschal(30), Siza Kanesa (22),Alex Daud(35), Oscar
Yosia (23), Traiphon Moasi (37) na Samson Mbwila(29).
Wengine
Veronica Elia (30),Dora Michael(35), Rabsen Ayub(26), Wasiwasi Spika (32), Asia
Anon(20),Bahati Kyando (23),Christopher Erasto(32) na Melisa Sanane (50)wote
wakazi wa kijiji cha Idweli.
No comments:
Post a Comment