Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, February 19, 2015

WAWILI WAFA,18 WAJERUHIWA WAKIIBA PETROLI

WATU wawili wamefariki dunia na wengine 18 kujeruhiwa vibaya baada ya kuungua na moto ulioripuka wakiwa wanajaribu kuiba mafuta aina ya petrol baada ya lori lililokuwa likisafirisha kupinduka.

Taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi mkoani Mbeya kwa vyombo vya habari zinaeleza kuwa walipoteza maisha katika ajali hiyo ni pamoja na mwanamke Maria Pajela(18) na Wiliam Pascal(38),wote wakazi wa kijiji  cha Idweli wilayani Rungwe.


Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi kupitia taarifa hiyo alisema  tukio hilo lilitokea jana(Feb18) majira ya saa tatu usiku katika kijiji cha Idweli, kata ya Isongole,  Tarafa ya ukukwe wilayani hapa.

 Kamanda Msangi alisema katika tukio hilo marehemu hao wawili kabla ya vifo vyao wakiwa na baadhi ya wakazi wengine wa kijiji cha Idweli walikuwa katika harakati za kuiba mafuta kutoka katika gari aina ya Scania  lenye namba za usajili T 891 AQZ likiwa na tela lenye namba T 821 ARF likitokea Dar es salaam kwenda nchini Malawi.


Amewataja majeruhi katika ajali hiyo ambao kati yao wanaume ni 13 na wanawake watano kuwa ni pamoja na Shukuru Kanzale (21),Nuru George (30), Asante Boniface(38), Joseph Jamson (18), Joseph Paschal(30), Siza Kanesa (22),Alex  Daud(35), Oscar Yosia (23), Traiphon Moasi (37) na Samson Mbwila(29).


Wengine Veronica Elia (30),Dora Michael(35), Rabsen Ayub(26), Wasiwasi Spika (32), Asia Anon(20),Bahati Kyando (23),Christopher Erasto(32) na Melisa Sanane (50)wote wakazi wa kijiji cha Idweli.

No comments:

Post a Comment