Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, February 3, 2015

ZIARA YA WAZIRI WA UJENZI DKT.JOHN MAGUFULI MKOANI MBEYA




Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli akisalimiana na mbunge wa Ileje Aliko Kibona wakati waziri huyo alipowasili wilayani Ileje kukagua barabara ya Mpemba Isongole inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.Wengine ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Mohamed Mwala(kushoto) na mkuu wa wilaya Rosemary Senyamule.
 
 Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli akikagua daraja la mto Songwe linalounganisha nchi ya Tanzania na Malawi kupitia mpaka wa Isongole wilayani Ileje alipokuwa ziarani wilayani hapo.Kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Ileje Rosemary Senyamule.



 


 Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli akishirikiana na maafisa kutoka wizara yake na viongozi wa halmashauri na wilaya ya Ileje kukata utepe kuzindua barabara ya Isongole-Itumba iliyojengwa na serikali kwa kiwango cha lami.



 Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli akipongezana na mbunge wa Ileje Aliko Kibona baada ya kuweka jiwe la msingi la uzinduzi wa barabara ya Isongole-Itumba iliyojengwa na serikali kwa kiwango cha lami.



 Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli akizungumza na wakazi wa mji wa Isongole wilayani Ileje alipokuwa katika ziara yake mkoani Mbeya.Akiwa Ileje Dkt Magufuli aliwahakikishia wakazi hao kujengwa kwa kiwango cha lami barabara ya Mpemba-Isongole na kubainisha kuwa serikali inaendelea kufanya mazungumzo na serikali ya Malawi ili kuona uwezekano pia wa barabara kutoka mpaka wa Isongole inajengwa kwa kiwango hicho upande wa Malawi.



 Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli akifurahia zawadi ya Mwiko na jamvi la asili aliyokabidhiwa na kikundi cha wanawake wajane wa wilayani Ileje.



 Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli akihutubia mamia ya wananchi wakazi wa Rujewa wilayani Mbarali katika mkutano uliofanyika mjini hapo,ajenda kubwa ikiwa ni ujenzi wa kipande chaa barabara kutoka Igawa hadi Ubaruku kinachoendelea kujengwa kwa kiwango cha lami ambapo serikali imesisitiza kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo ili kuwezesha mpunga unaozalishwa kusafirishwa.




Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli akishirikiana na mbunge wa Mbarali Dickson Kilufi kukata utepe kuzindua barabara ya Igawa-Ubaruku wilayani Mbarali inayoendelea kujengwa kwa awamu kwa kiwango cha lami


Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Joachim Nyambo akiwa pembezoni mwa daraja la Mto Songwe linalotenganisha nchi za Tanzania na Malawi kupitia mpaka wa Isongole wilayani Ileje.
 Mbunge wa Ileje Aliko Kibona akicheza ngoma ya asili iliyopigwa na moja ya vikundi vya sanaa wilayani Ileje
 Mkuu wa wilaya ya Ileje Rosemary Senyamule akizungumza jambo kabla ya kumkaribisha waziri wa Ujenzi kuhutubia wananchi.

 Watoto wataalamu wa mashairi ya kujigamba wakionesha kazi yao mbele ya waziri alipokuwa wilayani Ileje.
 Dkt.Magufuli akisalimiana na makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbarali mara baada ya kuwasili wilayani hapo.


Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Hussein Kandoro akizungumza jambo mbele ya wakazi wilayani Mbarali kabla ya kumkaribisha waziri kuhutubia.


No comments:

Post a Comment