Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro(wa tatu kutoka kushoto) akiwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Katiba,Sheria na Utawala kabala ya wajumbe hao kutembelea walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii(TASAF) wilayani Mbarani mkoani humo.Kulia ni mkurugenzi wa ukaguzi wa Tasaf Christopher Sanga.
MKuu wa wilaya ya Mbarali Gulamhussein Kifu(wa nne kulia)
akiwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Katiba,Sheria na
Utawala kabla ya wajumbe hao kutembelea walengwa wa Mpango wa kunusuru Kaya
Masikini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii(TASAF) wilayani Mbarani
mkoani humo.
Mwenyekiti
wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Katiba,Sheria na UtawalaVedastus Rweyikiza
akizungumza jambo baada ya kamati hiyo kukutana na wanufaika wa Mpango wa
kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii(TASAF) katika
kijiji cha Madabaga wilayani Mbarani mkoani Mbeya.
Wanufaika wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini
unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii(TASAF) katika kijiji cha Madabaga
wilayani Mbarani mkoani Mbeya wakimsikiliza mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya
Bunge ya Katiba,Sheria na Utawala Vedastus Rweyikiza kabla ya kuanza kugawiwa
fedha kwenye mkutano uliofanyika kijijini hapo jana.
Mmoja wa wanufaika wa Mpango wa kunusuru Kaya
Masikini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii(TASAF) katika kijiji cha Madabaga
wilayani Mbarani Hellena Bamba akikabidhiwa fedha kutoka kwa kamati ya mradi ya
wilaya(CMC).
Baadhi
ya wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Katiba,Sheria na Utawala wakiangalia
namna wanufaika wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini unaoratibiwa na Mfuko wa
Maendeleo ya jamii(TASAF) katika kijiji cha Madabaga wilayani Mbarani
wanavyokabidhiwa fedha.Katikati ni Mwenyekiti wa kamati hiyo Vedastus Rweyikiza
kushoto kwake akifuatiwa na Felix Mkosamali na Willium Ngeleja.
Mmoja wa wanufaika wa mpango akielezea manufaa aliyoyapata baada ya kuanza kuhamilishiwa fedha.
Wajumbe wa kamati ya bunge wakiwaaga wanufaika wa mpango katika kijiji cha Madabaga wilayani Mbarali mmkoani Mbeya.
HABARI KAMILI
WAJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Katiba,Sheria na Utawala wameonesha kuridhishwa na utekelezaji wa Mpango wa
Kunusuru kaya Masikini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii(TASAF) wilayani
Mbarali mkoani Mbeya.
Wajumbe wameonesha kuridhishwa na utekelezaji wa
mpango huo,baada ya jana kukutana na walengwa na kufanya mahojiano nao ambapo
wengi wa wa wanufaika walibainisha namna ambavyo fedha walizohawilishiwa
zimewaletea mabadiliko kimaendeleo.
Katika maelezo yao mbele ya wajumbe wa kamati ya
bunge, baadhi ya walengwa wameeleza namna walivyonufaika na fedha
zilizokwishatolewa ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto,kuboresha makazi yao na
kuwa na uhakika wa kupata huduma za afya na lishe.
Baadhi ya wanufaika Hellena Bamba,Amina January na
Spedito Kinyaga wamesema mpango wa kunusuru kaya masikini umewawezesha pia
kuanza kumudu maisha yao kwani wameweza pia kupata elimu ya kujikomboa kiuchumi
kwa kujihusisha na shughuli kama za ufugaji kuku na kilimo cha kisasa japo kwa
mashamba madogo madogo.
Akizungumza kwenye mkutano uliofanyika kijijini Madabaga,mwenyekiti
wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Katiba,Sheria na Utawala Vedastus Rweyikiza amewahimiza
wananchi hao kutumia fursa hiyo kwa ukamilifu ikiwa ni pamoja na kubuni miradi
itakayowafanya wawe katika mazingira mazuri hata baada ya mpango huo
kumalizika.
Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji wa
Tasaf Ladslaus Mananga,mkurugenzi wa ukaguzi wa mfuko huo,Christopher Sanga
alibainisha kuwa jitihada za kuwafikia walengwa wote wa mpango huo zinaendelea
ambapo ifikapo katikati ya mwaka huu zaidi ya kaya milioni moja zitanufaika na
utaratibu wa uhawilishaji fedha nchini kote.
No comments:
Post a Comment