Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, March 17, 2015

SERIKALI KUKIFUNGA KIWANDA CHA SUNSHINE MINING CHUNYA


 Waziri wa chi ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk.Binilith Mahenge akiwasikiliza raia wa China ambao ni viongozi wa Kiwanda cha Sunshin Mining ambao muda mwingi raia hao wawili ambao haikufahamika nani ni bosi kwa mwenzake walitumia zaidi lugha ya kichina kuliko kingereza kila walipoulizwa jambo.


 Waziri wa chi ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk.Binilith Mahenge akionesha namna miti iliyopo ndani ya bwawa ilivyokauka kutokana na sumu iliyopo kwenye maji yanayotoka kiwandani.
 Sehemu ya msitu wa asili ambao miti yake imekauka kutokana sumu ya maji kutoka kiwanda cha kampuni ya Sunshine Mining
 Sehemu ya msitu wa asili ambao miti yake imestawi kutokana na kutokuwa ndani ya bwawa la maji yenye sumu
 Wanahabari wakipiga picha bomba linalotiririsha maji kutoka kiwanda cha unhenjuaji dhahabu kinachomilikiwa na kampuni ya Sunshin Mining

Eneo zinakoishia taka za vyoo likiwa limejengwa kiholela huku pia likifunikwa juu kinyume na utaratibu wa utunzaji wamzingi katika maeneo ya migodi na viwanda unavyoelekeza. 

                              HABARI KAMILI

SERIKALI imetishia kukifungia kiwanda cha uchenjuaji dhahabu kinachomili kiwa na kampuni ya Sunshine Mining kilichopo wilayani Chunya iwapo uongozi wa kampuni hautafanyia kazi mapungufu yaliyopo kiwandani hapo.

Waziri wa chi ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk.Binilith Mahenge alitoa muda huo wa marekebisho alipotembelea na kujionea mapungufu kadhaa yaliyopo ikiwa ni pamoja na kiwanda kutoajiri afisa mazingira.

Mapungufu mengine yaliyopo ni kampuni kutojenga bwawa kwaajili ya kuhifadhia maji machafu yanayotoka kiwandani yakiwa yanaambatana na kemikali aina ya Sodium Cyanide ambayo inaathari kubwa katika afya ya viumbe hai ikiwemo binadamu.

Badala yake kampuni hiyo imejenga ukuta mnne wa kifusi na kuzuia moja ya mabonde ambayo ni chanzo cha maji yam to Lupa na kutumia sehemu ya bonde hilo kuwa bwawa la kuhifadhia maji machafu hali iliyosababisha pia viumbe hai ikiwemo miti kukauka kufuatia kemikali na kwakuwa bwawa hilo halijsakafiwa chini.

Kasoro hizo ndizo pia zilisababisha Julai mwaka jana maafisa wa Barza la Usimamizi wa mazingira nchini(NEMC) kukifungia kiwanda hicho lakini baada tu ya maofisa hao kuondoka uongozi ulikiuka na kuendelea na shughuli za uzalishaji kama kawaida.

No comments:

Post a Comment