Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, August 6, 2015

LUKUVI AWAKABIDHI MAAFISA ARDHI WATATU KWA TAKUKURU

WAZIRI wa Ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi Willium Lukuvi amewakabidhi mikononi mwa Tasisi ya kuzuia na kupambana na  Rushwa(TAKUKURU) maafisa wawili wa Idara ya Ardhi wa halmashauri ya jiji la Mbeya na mmoja kutoka ofisi ya wizara yake wanaokabiliwa na tuhuma za kujimilikisha viwanja 25 kinyume cha sheria.

Agizo la Lukuvi limekwenda mbali zaidi kwa kuwasimamisha kazi maafisa hao ili kupisha uchunguzi dhidi yao,uchunguzi ambao pia utahusisha tuhuma zinazowahusu za kubadili matumizi ya Eneo la viwanja la viwanda la Iyunga jijini hapa na kuwauzia wateja kama viwanja vya makazi.

Lukuvi ametoa agizo la kukamatwa kwa maafisa hao jana Agosti 5 ambapo amewataja kuwa ni pamoja na afisa ardhi mwandamizi wa jiji la Mbeya Ntala Castor na msaidizi wake James Venant Francis huku akimtaja kwa jina moja la Mwandoloma afisa ardhi aliyekuwa kwenye halmashauri hiyo kabla ya kuhamishiwa wizarani.

Waziri huyo amesema uchunguzi unaonesha maafisa hao walitumia vibaya mazoezi ya ugawaji wa viwanja vilivyopimwa kwenye maeneo ya Iwambi na Itezi kujinufaisha kwa kujigawia wenyewe viwanja vingi ambapo kati yao wapo waliojimilikisha zaidi ya viwanja kumi.

Amesema hesabu ya viwanja 25 walivyojigawia maafisa hao watatu ni vile tu vilivyoandikwa majina yao lakini zipo tetesi kuwa vipo viwanja vingine ambavyo ni vya kwao lakini walitumia ujanja wa kubadili majina.

Lukuvi amesema kwa ujumla maafisa ardhi wengi nchini wamekuwa wakiisababishia lawama serikali kwa wananchi kutokana na wengi wao kuwa na utendajikazi wenye kuendana na tama ya kujilimbikizia mali jambo ambalo limekuwa likiwasababishia wananchi adha kubwa.

Amesema suala la maafisa kujigeuza madalali wa kujimilikisha viwanja na kisha kuviuza viwanja hivyo kwa wateja kwa bei za juu halikubaliki na wanaobainika kama maafisa hawa wa jijini Mbeya watapewa adhabu ili kuwa mfano kwa wenzao.

No comments:

Post a Comment