Waziri mkuu Mizengo Pinda
akisalimiana na Meneja mashamba wa kampuni inayojishughulisha na masuala ya
kilimo ya Buyuni Redd Farms(T) Ltd Segundwa Lesilwa katika banda la kampuni
hiyo kwenye maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini.Kulia kwa waziri
mkuu ni Naibu waziri wa Kilimo,chakula na Ushirika Godfray Zambi na mke wa
waziri mkuu Mama Tunu Pinda.
Waziri
mkuu Mizengo Pinda na mkewe mama Tunu Pinda wakiangalia mchele uliosindikwa na
kufungwa katika vifungashio vya kisasa kazi inayofanywa na kampuni ya Mtenda
Kyela Rice Supply ya mkoani Mbeya
Mmoja wa wajasiriamali mkoani Mbeya
Allan Mwaigaga ambaye sasa ni wakala wa usambazaji wa Trekta zinazozalishwa na
kampuni ya Toyota akizungumza na wadau wa kilimo waliotembelea banda lake
kwenye maonesho ya wakulima ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini
akihamasisha vijana kuwekeza katika kilimo badala ya kupenda maisha ya kifahari
kwa kununua magari ya gharama.
Waziri mkuu Mizengo Pinda na
viongozi wengine wakimwangalia mbwa aliyefundishwa kufanya shughuli mbalimbali
kama binadamu ikiwemo kubeba mizigo.Mbwa huyo alikuwa kivutio kikubwa katika
maonesha ya wakulima Nanenane kanda ya nyanda za juu kusini yaliyofanyika kwenye
viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.
Mbwa aliyefundishwa kufanya shughuli
mbalimbali ikiwemo kubeba mizigo akiwa amebeba begi dogo ndani ya viwanja vya
maonesho ya Nanenane vya John Mwakangale
Kijana
ambaye hakufahamika jina wala makazi yake mara moja akiwa mikononi mwa vijana
wa Skauti wakimpeleka kituo kidogo cha polisi cha nanenane baada ya kumuokoa
mikononi mwa wananchi waliokuwa wakimpiga wakimtuhumu kuiba simu ya kiganjani
siku ya kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima Nanenane kanda ya nyanda
za juu kusini.
No comments:
Post a Comment