Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, September 11, 2013

MAITI YA KICHANGA YAOKOTWA KWENYE KITUO CHA MAFUTA

MAITI ya mtoto mchanga mwenye umri wa siku moja imeokotwa ikiwa imetelekezwa katika mji mdogo wa Tukuyu wilayani Rungwe. Maiti ya mtoto huyo mwenye jinsi ya kike imeokotwa jana(Septemba 10) mwaka huu majira ya saa nane mchana katika mtaa wa Bagamoyo nyuma ya kituo cha mafuta cha Caltex kilichopo mtaani hapo. Kamanda wa polisi mkoani hapa Diwan Athuman amesema leo kuwa mwili huo ulikuwa umeviringishwa kipande cha kitenge na kisha kuwekwa kwenye mfuko wa plastic maarufu kama Rambo. Kamanda Athuman amesema juu ya mfuko huo liliwekwa jiwe hali iliyodhihirisha mama wa mtoto huyo ambaye hajafahamika alimuua mwanaye baada ya kujifungua. Amesema jeshi la polisi linaendelea na msako ili mama wa mtoto huyo aweze kuchukuliwa hatua stahiki kutokana na tukio la kinyama alilotenda.

No comments:

Post a Comment