Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, September 3, 2013

WAPENDEKEZA KUBORESHWA KWA BAADHI YA IBARA ZILIZOPO KWENYE RASIMU YA KATIBA MPYA YA TANZANIA

WAKAZI wialayni Sumbawanga mkoani Rukwa wamependekeza kufanyiwa marekebisho kwa ibara ya 72,ibara ndogo ya 5 na 6 sehemu ya A na B ya rasimu ya katiba mpya ambapo tume imependekea rais anapofariki nafasi yake ichukuliwe na mgombea aliyeshika nafasi ya pili kwa wingi wa kura katika matokeo ya uchaguzi uliomweka madarakani. Wakichangia maoni yao kwenye mdahalo wa kupitia na kujadili rasimu hiyo ulioandaliwa na asasi ya vikundi vya wakulima wadogo wilayani Humo(Umawawa) uliofanyika katika kata ya Kaengesa baadhi ya washiriki wamesema kuwa uwepo wa ibara hiyo unaweza kusababisha mshindi wa pili kwenye uchaguzi husika kufanya njama za kumuua rais kwa tamaa ya kushika madaraka baada ya kifo. Mmoja wa wachangia hoja hiyo Fulgency Songoro amesema amependekeza katiba kutoa fursa ya kufanyika kwa uchaguzi mpya iwapo itatokea rais aliyepo madarakani amefariki dunia akisema hiyo italeta usawa wa kidemokrasia kwa wananchi kutumia masanduku ya kura kuchagua kiongozi wanayemtaka. Songoro pia amependekeza,pamoja na kubaki ikulu wakati wa kampeni za uchaguzi,katiba pia isimpe fursa rasi ya kutoa tamko lolote linalohusiana na uchaguzi badala yake aendelee na majukumu yake kama kawaida.

No comments:

Post a Comment