Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, September 21, 2013

T.PRISONS YATOSHANA NGUVU NA MTIBWA SUGAR.SHABIKI WAJIKUTA WAKO SOKOINE MBEYA WANASHANGILIA MECHI YA DAR ES SALAAM KATI YA MBEYA CITY NA SIMBA SC

Kwa mara nyingine tena timu ya Tanzani Prisons ya mkoani Mbeya imejikuta ikuibanwa mbavu baada ya kulazimisha sare ya goli 1-1 na Mtibwa Sugar ya Morogoro katika mchezo baina ya timu hizo uliopigwa kwenye uwanja wa Sokoine. Mtibwa Sugar pasipo kuonesha udhaifu wa kuwa ugenini ndiyo waliotangulia kupata goli lao katika dakika ya 26 kipindi cha kwanza likifungwa na Shaaban Nditi kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Said Mkopi na goli hilo kudumu hadi timu hizo zinakwenda mapumziko. Kipindi cha pili Tanzania Prison wakaonyesha uhai zaidi ya ule wa kipindi cha kwanza kwa kucheza mpira ambao ulionekana kuanza kuwakuna mashabiki wachache waliofika uwanjani hapo na hatimaye mnamo dakika ya 53 Peter Michael akamalizika kazi nzuri iliyofanywa na Jimmy Shoji aliyempa pasi iliyojaa ufundi na kuiandikia timu hiyo goli la kusawazisha. Hata hivyo katika kipindi hicho Tanzania Prisons watapaswa kujilaumu kwa kushindwa kutumia nafasi za wazi ilizopata ikiwemo ile iliyopatikana mnamo dakika ya 60 ambapo mshambuliaji Jeremiah Juma alibaki na mlinda mlango wa Mtibwa lakini akajikuta anapiga mpira ambao haukuweza kuleta madhara baada ya mlinamlango wa mtibwa kupangua shuti lake. Hata hivyo Mtibwa Sugar nao watapaswa kumshukuru mlina mlango wao Hussein Shariif kwani licha ya safu ya ushambuliaji ya wapinzani wao kuwa butu pia alifanya kazi ya ziada kuokoa mipira mingi hususani katika dakika za mwisho za mchezo ambapo Tanzania Prisons ilipiga kambi langoni kwake. Jambo lililokuwa kichekesho kikubwa uwanjani hapo ni kuona watazamaji wengi waliofika uwanjani wakionekana kujikita zaidi katika kusikiliza matangazo ya moja kwa moja ya mchezo kati ya Mbeya City ya jijini hapa na Simba ya Dar es salaam uliopigwa Dar es salaam na kujikuta mara kadhaa wakishangilia kila timu hiyo ilipotangazwa kufanya vizuri na kujisahau kama walikuwa uwanjani hapo kutazama mchezo wa Prisons na Mtibwa Sugar. Hadi kipenga cha mwisho cha mwamuzi Zhacharia Jackob kutoka mkoani Pwani kinapulizwa Tanzania Prisons moja ya Mbeya,Mtibwa Sugar moja.

No comments:

Post a Comment