Friday, September 27, 2013
KASANGA WANYAKUA MILIONI MOJA YA MASHINDANO YA NGOMA ZA ASILI
KIKUNDI cha ngoma cha Kasanga maarufu kama Ing’oma cha wilayani Rungwe kimeibuka mshindi katika mashindano ya ngoma za asili yaliyoandaliwa na kampuni ya bia ya TBL kupitia kiwanda chake cha Mbeya.
Mashindano hayo yaliyofanyika katika viwanja vya chuo cha uhasibu(TIA) jijini Mbeya yalishirikisha vikundi 26 vya Ngoma kutoka wilaya za Mbeya,Rungwe,Kyela,Mbozi,Njombe na Iringa.
Kwa ushindi huo kikundi cha Kasanga kilijinyakulia kitisha cha fedha taslimu shilingi milioni moja na kikombe.
Nafasi ya msindi wa pili ilikwenda kwa kikundi cha Lipango kutoka kata ya Isansa wilayani Mbozi ambacho kilizawadiwa fedha taslimu shilingi laki tano.
Nafasi ya tatu ilikwenda kwa kikundi cha Mbeta kutoka Isyesye jijini Mbeya ambacho kilizawadiwa shilingi laki mbili wakati vikundi vingine shiriki vilipewa kifuta jasho cha shilingi 50,000 kila kimoja.
Mkuu wa matukio wa kampuni ya TBL kanda ya Mbeya, Geophray Mwangungulu alisema lengo la mashindano hayo ni kuhamasisha wananchi kupenda ngoma za asili pamoja na utamaduni wao.
Mwangungulu alisema kumekuwepo na tabia ya baadhi ya watanzania kusahau asili zao kutokana na ujio wa sayansi na teknolojia hatua inayohitaji wadau kufikiri namna nzuri ya kuwezesha utamaduni wa makabila ya kiafrika kudumishwa.
Alitaja nyimbo na ngoma za asili kuwa miongoni mwa mambo muhimu yanayoweza kuiwezesha jamii ya kiafrika kuzikumbuka na kudumisha mila zao katika kipindi hiki ambacho tamaduni za kimagharibi zinaonekana kuenea kwa kasi katika mataifa mengi duniani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment