Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, September 2, 2013

MTOTO AGONGESHWA UKUTANI AFARIKI DUNIA

WATU wawili wamefariki dunia katika matukio tofauti mkoani Mbeya akiwemo la mtoto kugongeshwa ukutani. Kifo cha mtoto huyo aliyefahamika kwa jina la Aines Zacharia mwenye umri wa miezi mine mkazi wa kijiji cha Ivuna wilayani Momba kilitokea Septemba mosi saa saba mchana alipokuwa akiendelea kupata matibabu katika kituo cha afya Kamsamba wilaya hapo. Kaimu kamanda wa polisi mkoani hapa Barakael Masaki alisema awali kulikuwa na ugomvi kati ya mama wa mtoto huyo aliyemtaja kwa jina la Priscar Willson aliyekuwa amembeba mgongoni na mumewe Steven Cletus. Alisema kufuatia ugomvi huo Cletus alimsukuma mwanamke huyo na ndipo wakajikuta wanamgongesha mtoto ukutani na kumsababishia jeraha kubwa kichwani na ndipo mtuhumiwa alipokimbilia kusikojulikana na anatafutwa. Katika tukio jingine mtu aliyefahamika kwa jina moja la Oscar anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 30 na 35 amefariki dunia baada ya kudondoka kutoka katika gari. Masaki alisema ajali hiyo ilitokea Septemba mosi saa 4:45 asubuhi maeneo ya Mabatini jijini Mbeya katika barabara ya Meta/stendi kuu na kutaja gari husika kuwa ni namba T 773 BNL iliyokuwa ikiendeshwa na Deston Kabissa(29) mkazi wa Sae jijini hapa. Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa Mbeya na kuwa dereva anaendelea kushikiliwa wakati uchunguzi zaidi juu ya ajali hiyo ukiwa unaendelea.

No comments:

Post a Comment